• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Ingiza kipato kwa kukodisha

Patricia Richard by Patricia Richard
September 3, 2018
in BIASHARA
0
Kanuni ya Pareto inavyokuza biashara
Share on FacebookShare on Twitter

Biashara ya ukodishaji ni moja kati ya biashara muhimu na kubwa zinzazofanywa na watu wengi duniani. Fasili ya ukodishaji ni kitendo cha kutumia mali ya mtu kwa malipo ya fedha au kumlipa mtu fedha baada ya kutumia mali yake kwa muda uliopangwa kama makubaliano baina ya mteja na mmiliki. Vipo vitu vingi duniani ambavyo vimekuwa ni kawaida kukodishwa kutoka kwa mmiliki kwenda kwa mteja wake. Baadhi ya vitu hivyo ni nyumba, vyombo vya usafiri na kumbi za starehe

Zipo fursa mbalimbali za kiuchumi na biashara zinazotokana na kukodisha . Inawezekana nyingine umezisikia na umewahi kuzifanya lakini pia yawezekana nyingine ndo ukaziona hapa. Hivyo jambo la muhimu ni kufuatilia kwa umakini na kuangalia biashara ipi itakufaa kulingana na uwezo wako wa kifedha lakini pia mazingira uliyopo, kwa sababu moja ya jambo kubwa katika kuanzisha biashara ni kuangalia mazingira uliyopo.

Baadhi ya fursa ya ukodishaji ni kama hizi zifuatazo:

Ukodishaji vitabu

Huduma hii ni nzuri hasa kwa maeneo ya mjini ambayo mfanyabiashara anaweza kuanzisha maktaba yake au duka la vitabu kwa ajili ya kukodisha na kuuza kwa wateja mbalimbali. Mara nyingi huduma za kukodisha huenda sambamba na upangaji wa muda wa kurudisha pamoja na mdhamini endapo mtu aliyekodi mali hiyo hatorudisha. Suala la kuzingatia ni kufanya utafiti kabla ya kuanzisha biashara yako hasa kwa kujua jamii inayokuzunguka ina uhitaji wa vitabu gani. Kama umezungukwa na shule au chuo basi ni vema kununua vitabu vinavyohusu taaluma.

Ukodishaji vifaa vya sherehe

Fursa hii imekuwa ikikua kwa kasi . Mwanzoni ilizoeleka kinachokodishwa kwenye sherehe ni muziki tu, lakini kadri ziku zinavyoenda zimeanzishwa kampuni mbalimbali kwa ajili ya sherehe huku zikishugulika kuanzia upambaji, muziki, chakula na vyombo, mwendesha hafla (MC), na hivyo kutengeneza fursa kubwa ya kujiingizia kipato. Sio lazima kuanza na vyote unaweza kuanza na kimoja hata kwa kuwa MC na baadae ukanunua muziki wako na kumuajiri DJ (Msimamia muziki).

Ukodishaji vyombo vya usafiri

ADVERTISEMENT

Hapa vyombo vya usafiri vinavyozungumziwa ni pamoja na magari, mabasi, magari ya mizigo, pikipiki na hata meli. Shughuli hii ni fursa kubwa katika maeneo mengi nchini, ambapo zipo kampuni mbalimbali ambazo zimekuwa zikijishughulisha na ukodishaji wa vyombo mbalimbali vya usafiri kwa ajili ya shughuli kama sherehe, misiba, utalii na mikutano. Biashara hii inahitaji umakini katika kuisimamia kwa sababu jambo kubwa litakalomfanya mteja kuvutiwa na vyombo vyako ni pamoja na kumhakikishia usalama wa kutosha, usafi pamoja na historia nzuri.

Ukodishaji nyumba na vyumba

Hii ni moja kati ya biashara kubwa zaidi kufanywa duniani kote. Watu wengi wameweza kuwekeza katika miji mikubwa kupitia majengo. Wapo wanaokodisha vyumba katika nyumba za kulala wageni, nyumba za kupangisha watu wa kawaida pamoja na kwa ajili ya ofisi. Fursa hii inahitaji mtaji wa kutosha kuendana na kiasi cha uwekezaji unaotegemea kuanza. Mara nyingi mjasiriamali anashauriwa kufanya utafiti kabla ya kuanzisha ujenzi kwa kuangalia kama biashara anayotaka kufanya inalipa au la kulingana na eneo husika.

Ujasiriamali na uwekezaji ni masuala yanayoenda sambamba na wapo wengi waliofamikiwa kupitia sekta hizi. Ni muhimu kuchukua tahadhari kabla na baada ya kuanzisha biashara yako ili kufikia malengo uliyojiwekea.

Tags: biasharauchumiujasiriamaliuwekezaji
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Ijue Boeing ya ATCL

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In