• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Maeneo yaliyotengwa rasmi yanawashinda nini wamachinga?

Patricia Richard by Patricia Richard
June 4, 2018
in BIASHARA
0
Machinga wapigwa stop kuuza barabarani
Share on FacebookShare on Twitter

Kadri siku zinavyozidi kwenda, ndio kunakuwepo na ongezeko kubwa la wafanyabiashara hapa nchini hasa katika miji mikubwa ya biashara kama vile Dar es salaam. Ongezeko hili mbali na kurahisisha upatikanaji wa bidhaa zenye uhitaji mkubwa sokoni pia limepelekea wafanyabiashara wengi kufanya biashara zao kiholela maeneo mbalimbali ya miji. Hata baada ya serikali kupitia mamlaka husika kufanya jitihada za kutenga maeneo mbalimbali maalum kwa biashara ndogondogo watu wengi wameendelea kukwepa sehemu hizo na kuamua kufanya biashara zao katika maeneo wanayopendelea wao.

Unaweza kujiuliza kwanini wafanyabiashara hawa wanafikia maamuzi haya? Maeneo waliotengewa hayawatoshi? Kwanini wanauza katika maeneo ambayo sio rasmi? Serikali inachukua hatua gani kisheria dhidi yao? Vipi kuhusu usalama wa wateja na mali zao?

Huenda ushindani uliopo sokoni unawakimbiza katika maeneo rasmi ya biashara. Ni kweli kuwa ni vigumu kumvutia mteja kama watu kumi mnafanya biashara moja. Labda ni sababu mojawapo inayowakimbiza wafanyabiashara hawa na kuwasukuma kwenda maeneo ambayo wanaweza kumudu ushindani. Lakini kufanya hivi kunatatua tatizo? Watahama mara ngapi? Na huko wanapohamia hakuna ushindani? Idadi ya wateja inaridhisha? Kwanini wasiweke nguvu zaidi kuboresha huduma zinazotolewa ili kuwa tofauti na wapinzani wao na kujiweka katika nafasi nzuri zaidi?

ADVERTISEMENT

Mbali na hivyo, wateja wengi huwa tunaamini kuwa, wafanyabiashara wanaofanya shughuli zao katika maeneo rasmi yaliyotengwa huuza bidhaa zao kwa bei ya juu kuliko wale ambao hufanya nje ya maeneo hayo. Hivyo ili kupunguza gharama wengi huishia kununua mahitaji yao nje ya maeneo hayo japokuwa inawezekana gharama ni ile ile. Wateja wengi huishia mitaani na ni asilimia ndogo tu ndio hufanya manunuzi yao katika maeneo rasmi. Mtazamo huu ukibadilika miongoni mwa wanajamii, huenda wafanyabiashara watapata motisha ya kuendesha biashara zao katika maeneo wanayopatiwa na serikali kwani watakuwa na uhakika wa wateja.

Vilevile, kodi pamoja na tozo mbalimbali zinazokuwepo katika maeneo haya kwa kiasi fulani nazo zimechangia wafanyabiashara kufanya shughuli zao nje ya sehemu hizi. Wafanyabiashara wengi ni wadogo hivyo wanashindwa kumudu gharama za pango kwani zinakuwa kubwa kwao hivyo wanaona ni bora wakafanye shughuli zao sehemu ambazo hazitowaumiza kifedha. Wengi wamekuwa wakilalamika kuwa mamlaka husika zimekuwa haziangalii hali ngumu ya maisha na zimekuwa zikiwatoza gharama kubwa hali ambayo imepelekea wengi kushindwa kukaa katika maeneo hayo.

Japokuwa kuna changamoto mbalimbali katika suala hili, yapo mazuri pia. Mfanyabiashara kuendesha shughuli zake katika maeneo rasmi kunamuondolea wasiwasi kwani usalama unakuwepo sio tu kwake yeye bali kwa wateja pia. Biashara zinaendeshwa katika mazingira ya usafi hivyo inaondoa mazingira hatarishi ya magonjwa. Kufanya biashara kwenye maeneo haya pia inatoa fursa kwa wafanyabiashara kujifunza na kuwa wabunifu katika shughuli zao. Hivyo mamlaka husika zinapaswa kuendelea kuwahamasisha wafanyabiashara kutumia maeneo haya kwani yamejengwa hususani kwa ajili yao.

 

Tags: biasharakodiserikaliwateja
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Thamani ya ufundi stadi isionekane baada ya kufeli

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In