Home FEDHABIMA Unachotakiwa kujua kupata bima bora

Unachotakiwa kujua kupata bima bora

0 comment 20 views

Sera za bima zinatofautiana kulingana na idadi ya watu, eneo, na aina ya bima. Hakuna sera maalumu katika bima lakini ubora wake unatofautiana.

Kwa Tanzania, suala la bima bado ni changamoto na elimu inatakiwa kutolewa zaidi kwa watu ili waelewe umuhimu wa bima za aina mbalimbali, bima ipi inawafaa, bima ipi si muhimu kwa sababu asilimia kubwa ya watu hawana bima, na asilimia ndogo ya watu wenye bima hawajui bima ipi ina umuhimu na ipi si muhimu kwao.

Hivyo zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo zinaweza kukusaidia kupata bima yenye sera bora:

  • Viwango vya bima siku zote hutegemeana. Pia vipengele vingine muhimu huwa ni umri, na namba ya watu watakaokuwepo katika mpango husika. Hivyo gharama huwa tofauti kutokana na aina ya bima.
  • Aina nyingi za bima hulipiwa mara kwa mara (mara nyingi kila mwezi au kila mwaka). Hivyo gharama mbalimbali na namna ya malipo hutofautiana kutokana na aina ya bima.
  • Kulipia fedha kidogo au nyingi sana kunaweza kusababisha utumie fedha nyingi.
  • Kulipia fedha nyingi humaanisha malipo makubwa lakini humaanisha pia kuwa unalipia ulinzi mkubwa usiouhitaji
  • Kulipia fedha kidogo kwenye bima husababisha kutumia fedha zaidi katika mambo mengi ambayo hayapo kwenye mpango wa bima husika.
  • Kuchelewesha malipo au kutokuwa na sera inayotakiwa kunaweza kupelekea malipo ya ziada ya ada na kutolipa malipo ya Premium kunaweza kupoteza sera yako.
  • Unaweza kuokoa fedha kwa kwa kupata sera ya juu iliyotengwa hakikisha tu uko tayari kulipia kulipia punguzo ikiwa dharura itatokea.
  • Watoaji wa bima watatoa ofa ya viwango vya chini katika baadhi ya bima kwa kushiriki katika programu ambazo zinapunguza hatari ya umiliki wako wa sera.
  • Bima nyingi hulipia madai yanayohusiana kwa mfano kama ni bima ya afya gharama za madai ya matibabu, bima ya mafuriko hulipia mafuriko n.k. Hata hivyo, sera za mwavuli zinafunika mapungufu katika sera zingine.
  • Mapato na akiba vikiwa juu zaidi bima inakuwa ya muhimu zaidi.

Kuna aina nyingi za bima ikiwa ni pamoja na bima ya afya, bima ya gari, bima ya moto, bima ya uhandisi, bima ya vifaa vya kielektroniki, bima ya usafirishaji wa mizigo, bima ya wafanyakazi, bima ya makazi, bima ya hatari (risk), bima ya biashara, bima ya wizi, bima ya bandari na nyingine nyingi.

Ni vyema kufanya utafiti kuhusu aina ya bima unayotaka, kuuliza maswali ya kutosha kwa wataalamu wa sekta hii ili kunufaika.

 

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter