• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Friday, September 22, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Nyuki wanavyoweza kukupa utajiri

Ufugaji wa nyuki unakuja na faida mbalimbali.

Leah Nyudike by Leah Nyudike
June 12, 2019
in UJASIRIAMALI
0
Nyuki wanavyoweza kukupa utajiri
Share on FacebookShare on Twitter

Wazo la kwanza ambalo watu wengi hupata wakisikia nyuki ni hatari kwa sababu ya tabia yao ya kuuma. Licha ya kufanya hivyo, nyuki wanatengeneza vitu vingi ambavyo vina faida na vikiuzwa vinaweza kuleta utajiri mkubwa. Watu hufuga nyuki kwa njia za asili na njia za kisasa. Kufuga nyuki kwa njia za asili huchukua muda kupata matokeo kuliko kufuga nyuki kwa njia za kisasa hivyo ikiwa unataka kufuga nyuki jitahidi kuelewa njia zote ili kufanya maamuzi sahihi.

Ufugaji nyuki una faida mbalimbali zikiwemo:

Asali

Hii ni moja ya bidhaa ambazo hutokana na nyuki na kupitia asali watu mbalimbali wametajirika. Inaelezwa kuwa kwa barani Afrika watu wanatumia asali mara tatu zaidi ya ile inayozalishwa hivyo watu wanatakiwa kuchangamkia fursa ya uzalishaji wa asali kwa sababu kuna soko la uhakika. Watu hufurahia kutumia asali kwa sababu imeshathibitishwa kuwa inaweza kutumika kama dawa kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali, vilevile inaweza kutumika katika chakula na uwekaji wa asali katika vitu husababisha vitu hivyo visiharibike ndio maana watu wengi huona umuhimu wa kununua asali kwa kuwa inaweza kutumika katika mambo mengi kwa mara moja. Hivyo ili kujipatia soko, unatakiwa kuwa makini na vifungashio vyako ili kuwavutia watu wa ndani na nje ya nchi kununua asali zako.

Nta

Wazalishaji wengi wa nyuki hutupa nta bila kujua faida wanayoweza kuipata kutokana na bidhaa hii. Nta kutumika katika mambo mengi sana ikiwa ni pamoja na katika viwanda vya usindikaji chakula, hutumika kutengeneza mishumaa, katika vipodozi kama mafuta. Pia hutumika kwenye polishi ya viatu na samani n.k. Uzuri wa nta ni kwamba huwa haiharibiki hivyo kila ukitaka kuitumia unaiyeyusha na kurudia tena hivyo mara nyingine. Hivyo kwa kuuza nta mzalishaji anakuwa na uhakika wa soko katika viwanda na hata kwa watu binafsi.

ADVERTISEMENT

Sumu ya nyuki (Bee Venom)

Nyuki hutengeneza sumu kwa ajili ya kujikinga na hatari. Lakini kwa upande wa binadamu sumu hiyo hutumika kuponya magonjwa. Hivyo  basi mfugaji nyuki anaweza kuongea na taasisi zinazojihusisha na masuala ya utengenezaji dawa kwa kutumia sumu hiyo na kuingia nao mkataba wa kufanya biashara.

Gundi

Nyuki hutumia gundi yao kurekebisha mizinga yao kwa kuziba sehemu zenye ufa ili wadudu au maji yasiingie ndani. Gundi hiyo hutumika kutibu magonjwa ya fangasi, vidonda vya tumbo, ngozi iliyoungua na hata magonjwa ya mlipuko. Ikiwa mtu amepata matatizo haya lazima ataenda kununua gundi kwa wazalishaji ili kuondokana na magonjwa hayo. Pia katika sekta ya afya lazima wanunue gundi hiyo ili kutengeneza dawa.

Maziwa ya nyuki

Haya hutengenezwa na nyuki vijakazi. Utafiti unaonyesha kuwa maziwa haya yana vitamini b na watu huyatumia kwa ajili ya kupata muonekano wa vijana huku ikielezwa kuwa maziwa haya huongeza nguvu za kiume. Mziwa haya yanatumika sana barani Asia kwa ajili ya dawa. China peke yake hutumia tani 75 kwa mwaka hivyo mfugaji wa nyuki anaweza kuchangamkia fursa hii na kuuza maziwa ya nyuki katika soko la kimataifa.

Watanzania hususani vijana wanatakiwa kuacha uoga kwenye suala la ufugaji wa nyuki na kuchangamkia fursa zilizopo ili kuleta maendeleo. Ni muhimu kusoma zaidi kuhusu ufugaji huu na pia kukutana na afisa maliasili ili kupata elimu zaidi na baadae kuwekeza katika ufugaji huu.

Tags: biasharaelimunyukisokoufugaji
Leah Nyudike

Leah Nyudike

Mwandishi

Next Post
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, Vodacom Tanzania, Jackline Materu akizungumza katika uzinduzi wa kampeni ya Data na AFCON kupitia huduma ya Soka Letu, hapo jana, Dar es Salaam. Kulia kwake ni  Afisa kitengo cha digitali na huduma za ziada, Furaha Limu na Kushoto ni Meneja wa Kitengo cha Vijana Abdi Zagar.

Vodacom kupeleka mashabiki wa Taifa Stars Misri

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

September 14, 2023

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

September 14, 2023
Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande.

Tanzania yapiga hatua utakatishaji fedha

September 12, 2023
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Picha| Ikulu

Tutawaunganisha wakulima na soko: Rais Samia

September 11, 2023

Mbaazi yaleta neema kwa wakulima 2023

September 7, 2023

Bei za mafuta zapanda tena Tz

September 6, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Tanzania ni nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali barani Afrika na inashika nafasi ya 14 dunia. Ethiopia, ndio nchi...

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Benki ya Exim imezindua ushirikiano wa kimkakati na Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na kufanya mafunzo ya...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In