• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Fahamu zaidi kuhusu kilimo cha tikiti maji

Patricia Richard by Patricia Richard
May 16, 2018
in KILIMO
0
Share on FacebookShare on Twitter

Kilimo cha tikiti maji kimekuwa kikijizolea umaarufu mkubwa hapa nchini. Wakulima wengi zaidi wamekuwa wakihamia kwenye kilimo hiki miaka ya hivi karibuni. Katika mijadala mbalimbali ya fursa za kilimo, kilimo hiki ni nadra sana kukosekana. Kama unafikiria kuingia katika aina hii ya kilimo, makala hii itakuelezea kwa undani kuhusiana na aina hii ya kilimo pamoja na faida na hasara zake.

Hapa Tanzania soko la tikiti maji ni zuri kipindi cha joto ambapo walaji wengi hupendelea tunda hili kutokana na hali ya hewa ya joto. Wauzaji wa matikiti katika masoko wanadai  kuwa biashara ya tikiti ni nzuri sana wakati wa joto na hudorora katika nyakati za baridi. Taarifa kama hizo ni nzuri sana kwa mkulima mjasiriamali anayelenga uhitaji wa soko kwani anakuwa na mipangilio mizuri katika uzalishaji wake ili asipate hasara.

Kwanza ni kilimo cha muda mfupi kwani huchukua miezi miwili hadi mitatu kiasi kwamba mkulima anaweza kulima hadi mara nne kwa mwaka mmoja. Kilimo cha tikiti maji kinafanyika katika eneo lenye udongo laini usio na mabonge kwani mbegu zake hupandwa moja kwa moja shambani. Pia shamba linapaswa kuwa katika eneo la wazi lisilo na miti sababu vivuli vya miti vinaweza kupelekea matikiti yasitoe matunda.

Uchaguzi wa aina ya mbegu ni kitu cha msingi sana katika kilimo hiki kwani shughuli zote zinajengwa kwenye msingi huo. kama ukikosea kuchagua aina ya mbegu  kilimo chako hakitakuwa na tija. Kuchagua mbegu nzuri na zenye ubora sio kazi rahisi, wakulima wengi hukimbilia mbegu maarufu ambazo zinatangazwa zaidi ambapo mara nyingi wanapokwenda kwenye uhalisia kwa kulima mbegu hizo, wanakumbana na matokeo tofauti.

Takribani asilimia tisini ya tikiti maji ni maji hivyo yanahitaji maji mengi ili kukua vizuri. Hivyo kabla ya kufanya aina hii ya kilimo, hakikisha una uhakika wa maji kipindi chote cha ukuaji. Matunda haya huitaji maji kipindi chote mpaka hatua ya uvunaji. Mizizi ya mmea wa tikiti huenda chini sana kutafuta maji kwa ajili ya kusaidia matunda yenye ukosefu wa maji. Mkulima anatakiwa kumwagilia mimea maji ya kutosha. Kama kiwango cha maji hakiridhishi basi hata matunda hayo hayawezi kukua kama inavyotakiwa.

ADVERTISEMENT

Hasara katika kilimo cha tikiti maji hutokea kwa kiasi kikubwa kwenye kipindi cha uvunaji. Wakati huu ukifika, mkulima anakuwa na shauku kubwa ya kutaka kuonja matikiti yake ili kuona yana ladha na ubora gani. Tatizo hutokea pale inapotakiwa kutenganisha matikiti yalioiva na yale ambayo bado hayajaiva. Wengi huharibu matikiti mengi kutokana na kukosa uelewa na ujuzi wa kutenganisha makundi hayo mawili hivyo hupata hasara kubwa wakati zoezi hili likifika.

Kama unafikiria kujiajiri kupitia kilimo biashara, kilimo cha tikiti maji ni njia mojawapo ya kufanya hivyo.unaweza kulima, kuvuna na kuuza hata mara nne ndani ya mwaka mmoja hivyo kujiingizia kipato kikubwa tu. Jambo la msingi ni kuwa na uelewa mkubwa kuhusiana na kilimo hiki na kuhakikisha kuwa umejiandaa vema na umejiwekea malengo. Hakikisha pia soko lako ni la uhakika na ka kufanya hayo lazima jitihada zako zitazaa matunda.

Tags: kilimoTikiti majiuzalishaji
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Kitendawili cha miundombinu vijijini mpaka lini?

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In