• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Naibu Waziri atamani kilimo kiwanufaishe wakulima

Mikakati kuinua zao la mkonge Tanzania

Pesatu Reporter by Pesatu Reporter
February 14, 2022
in KILIMO
0
Mkonge ni miongoni mwa mazao ya kimkakati nchini.

Mkonge ni miongoni mwa mazao ya kimkakati nchini.

Share on FacebookShare on Twitter

Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde amefanya ziara ya kikazi mkoani Tanga ambapo amezungumza Menejimenti ya Bodi ya Mkonge Tanzania baada ya kukagua ukarabati wa jengo la ofisi ya Bodi hiyo.

“Natamani kuwaona wakulima nchini wakinufaika kwa kazi wanayoifanya”, amesema Naibu Waziri.

Mavunde amesema Serikali ina malengo ya kukuza uchumi wa kaya na uchumi wa mtu mmoja mmoja kupitia zao la mkonge.

ADVERTISEMENT

“Moja ya malengo ambayo serikali tumejiwekea ni kulipa kipaumbele zao la mkonge ambalo ni moja ya mazao ya kimkakati na tutahakikisha tunaisaidia Bodi ya Mkonge kutimiza wajibu wake ili uzalishaji uongezeke mkulima anufaike na zao hili”, amesema Mavunde.

“Nitoe rai kwa wananchi mkoa wa Tanga na maeneo yote yanayolima mkonge nchini, niwaombe muendelee kuiamini bodi yetu na kufanya nayo kazi na mjitokeze kwa wingi sana kwenye kilimo hiki, najua mlikuwa na changamoto nyingi sana ikiwemo mkonge mwingi kubaki shambani hauvunwi kwa sababu ya uwepo wa makorona mengi ya kusaidia uvunwaji”.

“Serikali tumedhamiria katika bajeti inayokuja na nimeshamuelekeza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge kuanza mchakato mara moja wa kutangaza zabuni ya kununua makorona mengine matatu kwa ajili ya kusaidia uchakataji ili pia tuwe tumerahisisha kwa wakulima kupata sehemu ya uhakika ya uchakatwaji wa mazao yao,” amesema Mavunde.

Saddy Kambona ambae ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania amesema amepokea maelekezo hayo na kusema ni hatua kubwa mbele katika kuchochea uzalishaji wa kilimo cha mkonge.

“Sisi bodi tutahakikisha mchakato huu unakwenda haraka makorona haya yaweze kununuliwa haraka zaidi. Kwa hiyo niwatie shime wananchi kuendelea kulima mkonge serikali iko pamoja nao,” amesema.

Naibu Waziri Mavunde ameitaka Menejimenti ya Bodi ya Mkonge kuleta matokeo chanya ya ukuaji wa uzalishaji wa zao la Mkonge kwa kuja na ubunifu utakaochochea kilimo hicho.

Amewasisitiza kutofanya kazi kwa mazoea na badala yake wahakikishe wanaacha alama katika kilimo cha Mkonge.

Katika ziara hiyo ya siku mbili iliyofanyika mwishoni mwa wiki Mavunde pia ametembelea Jengo la Ofisi za Bodi ya Mkonge Tanzania, kiwanda cha kutengeneza bidhaa za mkonge ambacho kinamilikiwa na Shirika la Hifadhi za Jamii (NSSF) na kusimamiwa na Kampuni Tanzu ya Sisalana, Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) na kuzungumza na wanachama wa vyama vya msingi vya ushirika (Amcos), vinavyolima mkonge mkoani Tanga.

Tags: biasharakilimoKilimo Biasharamkonge
Pesatu Reporter

Pesatu Reporter

Next Post

Vilio vya wafanyabiashara masoko kuungua moto

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In