• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, January 29, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Unakifahamu vizuri kilimo cha umwagiliaji?

Patricia Richard by Patricia Richard
May 16, 2018
in KILIMO
0
Kilimo cha umwagiliaji: Mambo muhimu ya kuzingatia
Share on FacebookShare on Twitter

Imezoeleka hapa nchini kuwa wakulima hutegemea kilimo cha mvua pekee, hali ambayo inawalazimu kulima kwa misimu. Wakulima wengi hawana uelewa kuhusu kilimo cha umwagiliaji hivyo mvua inakuwa chanzo pekee cha wao kupata maji ya uhakika. Mbali na kutokuwa na elimu ya kutosha kuhusu aina hiyo ya kilimo, wakulima wengi pia huchagua kuamini kuwa kilimo hicho hufanywa na watu wenye uwezo mkubwa kifedha, jambo ambalo halina ukweli wowote.

Kabla ya yote ni vizuri kufahamu kilimo cha umwagiliaji ni nini? Hiki ni kilimo ambacho maji kutoka vyanzo vingine hupelekwa kwenye mmea, kwa maana hiyo kilimo cha umwagiliaji hakitegemei maji ya mvua pekee. Mkulima anaweza kupata maji kutoka mtoni, ziwani au kwa kufunga pampu ambayo inavuta maji kutoka kisimani au sehemu yoyote yenye maji ya uhakika. Kupitia aina hii ya kilimo, mkulima anapata uhakika wa maji katika shughuli zake hivyo hata uzalishaji nao unakuwa wa uhakika kipindi chote cha mwaka.

ADVERTISEMENT

Kuna aina mbalimbali za kilimo cha umwagiliaji lakini kwa hapa nchini njia hizi nne ndiyo hutumika zaidi. Umwagiliaji unaweza kuwa katika njia ya mafuriko (Surface Irrigation), njia ya matone (Drip Irrigation), njia ya mtawanyo (Sprinkler Irrigation) na mwisho ni njia ya mabomba (Sub surface Irrigation). Mara nyingi njia ya mtawanyo hutumika katika mashamba makubwa wakati njia za matobe, mafuriko na mtawanyo hutumika zaidi na wakulima wadogo wadogo.

Wadau mbalimbali wa masuala ya kilimo kama vile Shirika la Maendeleo la Watu wa Japan (JICA) pamoja na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AFDB) pamoja na taasisi nyingine wamekuwa wakijitahidi kuhamasisha kilimo hiki hapa nchini. Nchi ya Japan imekuwa ikitoa misaada kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha Umwagiliaji hapa nchini tangu mwaka 1970. Mbali na uwepo wa taasisi kama hizi ambazo zimekuwa zikijitolea kifedha, pia kuna zile ambazo zimekuwa zikitoa elimu juu ya kilimo cha umwagiliaji kupitia mikutano na program mbalimbali kwa lengo la kubadilisha mtazamo walionao wakulima wengi juu ya kilimo hicho.

Japokuwa jitihada zote hizi zimekuwa zikifanyika, aina hii ya kilimo imekuwa na changamoto mbalimbali kwa hapa nchini. Baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na ukosefu wa mifumo bora ya kuendeleza kilimo hicho, vihifadhi bora vya maji kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya kilimo cha umwagiliaji pia ni changamoto kubwa, upungufu wa wataalamu wa kutosha katika halmashauri na wilaya nao unarudisha nyuma kilimo hiki kwa kiasi kikubwa.

Asilimia kubwa ya watanzania wamejiajiri au wameajiriwa kupitia kilimo. Kuna kila sababu ya wadau wa kilimo kutoa elimu stahiki kuhusu kilimo cha umwagiliaji na faida zake ili watanzania wabadilike na kuanza kufanya kilimo cha kisasa zaidi.

Tags: elimukilimoumwagiliajiwakulima wadogo
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Mbinu za kukuza biashara ya chakula

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In