Serikali ya Tanzania imetangaza ajira 21,200 kwa kada za walimu na afya.
Tangazo la Serikali limetolewa na Waziri wa TAMISEMI Angella Kairuki April 12, 2023 Jijini Dodoma ambapo amesema mwisho wa maombi hayo ni tarehe 25 April, 2023 saa 05:59 usiku.
Waziri Kairuki ametaja mgawanyo wa nafasi hizo ni 13,130 ambazo zitachukuliwa na walimu wa shule za msingi na Sekondari.
Aidha idadi ya watumishi watakaoajiriwa katika kada za Afya ni 8,070 ambao watafanya kazi katika Hospitali za Halmashauri, Vituo vya Afya na Zahanati.
Waombaji ni wahitimu wa nafasi hizo kuanzia mwaka 2015 hadi 2022 ambao watakuwa na sifa stahiki na wasiozidi umri wa miaka 45 lakini wanaofanya kazi za kujitolea wameitwa kuomba nafasi hizo ili waingie katika mfumo wa ajira serikalini.