Home HABARI ZA AFRIKA MASHARIKI Ushuru vifaa mahitaji maalum watolewa

Ushuru vifaa mahitaji maalum watolewa

0 comment 81 views

Serikali imesema kuwa inatoa msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) na ushuru wa forodha kwenye vifaa vilivyotengenezwa mahususi kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Hamad Hassan Chande (Mb) alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Grace Victor Tendega aliyetaka kujua utayari wa Serikali kuondoa kodi kwenye vifaa vinavyotumiwa na watu wenye ulemavu wakati wa kuingia nchini.
Chande amesema msamaha wa kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) umeainishwa katika kipengele cha nane (8) na 12 (d) cha Jedwali lililopo kwenye Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani, SURA 148.

“Vifaa vilivyopewa msamaha wa kodi ni pamoja na baiskeli na magari yaliyotengenezwa mahususi kwa matumizi ya Watu Wenye Ulemavu”, amebainisha Naibu Waziri.

Ameongeza kuwa Serikali inatoa msamaha wa VAT kwenye huduma za elimu zinazotolewa katika vituo vya mafunzo ya mwili na akili kwa watu wenye mahitaji maalum.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter