Home WANAWAKE NA MAENDELEO Wanawake washauriwa kutumia vizuri fursa za ujasiriamali

Wanawake washauriwa kutumia vizuri fursa za ujasiriamali

0 comment 64 views

Mkurugenzi wa Taasisi ya New Vision Consortium (NVCT) Pily Khamis Lapda ametoa wito kwa wanawake wa visiwani Zanzibar kutumia vizuri fursa ya ujasiriamali ili kujiongezea kipato na kufanikiwa kujiajiri. Lapda ameeleza kuwa asilimia kubwa ya wanawake wamekuwa wakifanya shughuli za ujasiriamali kwa mazoea na hivyo kushindwa kufikia malengo yao.

Amesema kuwa kuna njia mbalimbali za kuwakomboa wanawake na ameshauri wanawake nchini kujiamini na kujiwekea malengo ya kudumu ya biashara ambayo yawasaidia kumiliki mitaji mikubwa ya kibiashara.

Taasisi ya NVCT imekuwa ikisimamia mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kitaalamu makundi  mbalimbali kwa lengo la kuwawezesha kuwa na uwezo wa kutumia fursa mbalimbali za ujasiriamali ili kuleta maendeleo. Mkurugenzi huyo amewataka wanawake kuwa mstari wa mbele kujifunza mbinu za kujikwamua kiuchumi na kuwa wabunifu ili kukuza biashara zao.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter