Home FEDHAMIKOPO Deni la Serikali ni Sh 82.12 trilioni

Deni la Serikali ni Sh 82.12 trilioni

0 comment 92 views

Waziri wa Fedha Dk Mwigulu Nchemba amesema hadi kufikia Juni 2023, deni la Serikali lilikuwa ni Sh 82.12 trilioni huku mikopo ikitumika kugharamia miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, viwanja vya ndege, umeme, afya na elimu.

Waziri Nchemba amesema hayo Novemba 6, wakati akiwasilisha mapendekezo ya mwongozo wa maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2024/25.

Amebainisha kuwa tathmini ya uhimilivu wa deni iliyofanyika Desemba 2022 inaonesha kuwa deni la Serikali limeendelea kuwa himilivu katika kipindi cha muda mfupi, wa kati na mrefu.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter