Home HABARI ZA AFRIKA MASHARIKIUJASIRIAMALI Mkuu wa wilaya awahamasisha vijana Mtwara

Mkuu wa wilaya awahamasisha vijana Mtwara

0 comment 51 views
Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Evod Mmanda amewataka vijana wilayani humo kuchangamkia fursa ya urasimishaji ujuzi inayotolewa na Mradi wa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi (YEE) kwa kufanya kazi kwa ushirikiano ili waweze kuondokana na tatizo la ajira nchini. Mmanda amesema mradi huo umekuwa ukiwapa ujuzi vijana kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi na kuwaongezea uwezo katika stadi mbalimbali ili waweze kujiajiri.

Mradi huu umepanga kugusa zaidi vijana wanaotoka katika familia zisizojiweza na wenye kipato kidogo hasa wasichana na walemavu ili kuwapatia nafasi ya kuboresha maisha yao na kuwawezesha kutumia ujuzi wao na kuleta tija ndani ya jamii.

Mratibu wa Mafunzo wa mradi huo Nurdin Amri amesema mpaka sasa vijana 1,500 wameshafikiwa katika Wilaya ya Mtwara. Mradi huu umelenga kuwezesha vijana kati ya miaka 15 hadi 35 ili kuwaepusha na mazingira hatarishi.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter