Home KILIMOKILIMO BIASHARA Serikali ya Tanzania yajipanga utafiti wa mazao

Serikali ya Tanzania yajipanga utafiti wa mazao

0 comment 66 views

Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde amewaeleza wadau wa vanila namna Serikali ilivyojipanga kufanya utafuti wa mazao likiwemo zao la vanila.

mavunde amesema hayo wakati akifungua mkutano wa Wadau wa Zao la Vanila nchini.

Amesema Vanila ni moja ya mazao yanayoweza kuwekewa mkakati ili kuongeza uzalishaji na uuzaji kwenye soko la kimataifa.

“Jambo kubwa ni kuhakikisha zao hili la vanilla liwe katika utaratibu mzuri kwa kutengenezewa muongozo ambao utatusaidia kujibu hoja nyingi sana ambazo zimewasilishwa hapa.

Tumefanya hivi katika mazao mengi sana ya mbogamboga na matunda, tumekamilisha mwongozo wa parachichi ambayo nayo ilikuwa changamoto kubwa, hamasa kwa wakulima ilikuwa ni kubwa lakini walikuwa wanakwenda bila kuongozwa na ilitupelekea kupata changamoto nyingi sana pamoja na kupata notification nyingi sana kama nchi ambazo zilikuwa pia zinaathiri soko letu la kimataifa la mazao ya kilimo,” ameeleza.

Asemema hali hiyo ilikuwa inaatarisha soko la Tanzania la mazao ya kilimo

Amesema moja kati ya changamoto kubwa ilikuwa ni mfumo wa mnyororo wa ubaridi wa uhifadhi mazao ya mbogamboga na matunda.

Kuhusu kutambulika kwa ubora wa mazao ya kilimo katika viwango vya kimataifa Mavunde amesema tayari Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viwatilifu (TPHPA) imeshapata ithibati za kimataifa ambayo inathibitisha ubora wa mazao kimataifa.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter