Home LifestyleTravel The Royal Tour imefanikiwa kwa kiwango kikubwa: Masanja

The Royal Tour imefanikiwa kwa kiwango kikubwa: Masanja

0 comment 101 views

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja amesema filamu ya “The Royal Tour” imefanikiwa kwa kiwango kikubwa na kwamba kwa sasa watalii wameongezeka.
Masanja ameyasema hayo alipotembelea maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam maarufu kama Sabasaba.

Filamu hiyo, ilizinduliwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

“Tunatambua kwamba ni nadra sana kumpata kiongozi anayeamua kuongoza kwa vitendo kama alivyofanya Rais Samia, ametangaza kwa vitendo vivutio vyetu hivyo tunatakiwa kuvitembelea ili kumuunga mkono,” amesisitiza Masanja.

Aidha, ametumia nafasi hiyo kuwahimiza Watanzania kutembelea vivutio vya utalii vilivyoko nchini akitolea mfano wa maeneo ya Malikale, Misitu ya Asili, tamaduni za Kitanzania, historia za Tanzania za Waasisi wa Taifa na maeneo mengine ya utalii.

“Tutembelee vivutio vyetu, ukishakitembelea kile kivutio unakuwa umechangia pato la Taifa lakini hata wewe mwenyewe utakuwa umejifunza historia ya nchi ilivyo lakini pia utapunguza hata msongo wa mawazo,” amesema Masanja.

Leave a Comment

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter