Home WANAWAKE NA MAENDELEO Sh milioni 200 zimetengwa majukwaa ya wanawake

Sh milioni 200 zimetengwa majukwaa ya wanawake

0 comment 84 views

Shilingi milioni 200 zimetengwa kwa ajili ya kugharamia majukwaa ya wananake kwa mwaka 2023/2024.

Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Exaud Kigahe amesema hayo jijini Dodoma wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum, Subira Mgalu wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Katika swali lake la msingi, Mgalu alitaka kujua ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya uendeshaji wa Mabaraza ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi.

Kigahe amesema Serikali imekuwa ikiendesha Majukwaa (siyo Mabaraza) ya Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi tangu mwaka 2017.

Amesema lengo kuu la Majukwaa hayo ni kuwakutanisha wanawake ili waweze kujadili fursa za kiuchumi na changamoto mbalimbali wanazokutana nazo wakati wa utekelezaji wa shughuli za kiuchumi nchini.

Amesema hadi kufikia mwaka 2021/2022, Mikoa yote 26 imezindua Majukwaa ya wanawake.

Amebaibisha kuwa katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali ilitenga zaidi ya Sh milioni 72 na kwa mwaka 2023/ 2024 imetenga Sh milioni 200 kwa ajili ya uendeshaji wa majukwaa hayo.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter