Home Elimu Sekondari zashauriwa kuanzisha klabu za historia

Sekondari zashauriwa kuanzisha klabu za historia

0 comment 108 views

Shule za Sekondari nchini zimeshauriwa kuanzisha klabu za Historia kwa ajili ya kujenga uelewa kwa wanafunzi juu ya historia ya nchi yao na uzalendo.

Ushauri huo umetolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Malikale nchini Dkt. Kristowaja Ntandu alipotembelea Mnara wa Kumbukumbu ya aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Hayati Edward Moringe Sokoine na kukutana na uongozi wa Shule ya Sekondari ya Kumbukumbu ya Sokoine, mkoani Morogoro.

Dkt. Ntandu ameeleza kuwa maeneo ya kihistoria ni mwalimu mzuri wa uzalendo, utu, umoja na mshikamano wa kitaifa hivyo yanapaswa kuhifadhiwa.

Naye Kaimu Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu, Hathuman Kilenja ameipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Idara ya Malikale, kwa kuona umuhimu wa kutembelea shule hiyo kuhamasisha uhifadhi wa eneo hilo muhimu na kuanzisha klabu ya historia.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter