Home BIASHARA Kampuni ya Urusi kununua matunda Tanzania

Kampuni ya Urusi kununua matunda Tanzania

0 comment 84 views

Kampuni ya Magnit ya nchini Urusi imeeleza nia ya kununua bidhaa mbalimbali kutoka Tanzania ikiwemo matunda.

Hayo yameelezwa katika mkutano ulioratibiwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) kati ya kampuni hiyo na kampuni za Tanzania.

Mwakilishi wa Kampuni hiyo ameeleza kuwa wanayo nia ya kununua bidhaa mbalimbali kutoka Tanzania ikiwemo ndizi, nanasi, embe, passion, papai na parachichi.

Bidhaa nyingine ni kahawa, korosho, alizeti, viazi na soya.

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Biashara kutoka TanTrade Emmanuel Miselya amewaeleza washiriki kuwa mkutano huo umelenga kuendeleza na kuimarisha mahusiano ya kibiashara kati ya Tanzania na Urusi.

Amewataka wafanyabiashara wa Tanzania kuchangamkia fursa za masoko kwa bidhaa zinazohitajika na kampuni hiyo ili kukuza uchumi wa nchi na kuendelea kunufaika na mahusiano mazuri baina ya nchi hizo mbili.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter