Virusi vya corona vinaweza kumuathiri mtu yeyote, lakini watu wenye maradhi fulani pamoja na wazee wapo hatarini zaidi kuambukizwa ugonjwa huo.
Iwapo umekuwa ukiugua kwa muda mrefu unaweza kutishiwa na habari hii. Lakini je ni nani aliye katika hatari ya kuambukizwa?
Wengi wa wale walio katika hatari ya maambukizi ni watu wenye umri wa miaka 70 kwenda mbele, wale wenye maradhi ya ubongo na watu walio chini ya umri wa miaka 70 iwapo wanakabiliwa na dalili zifuatazo.
- Magonjwa ya mapafu kama vile pumu, uchungu mkali kifuani , kushindwa kupumua na kuwa na homa kali.
- Magonjwa ya moyo, ikiwemo mshtuko wa moyo
- Maradhi ya figo
- Maradhi ya ini
- Shinikizo la akili
- Kisukari
- Maradhi ya utumbo kwa mfano anapofanyiwa
- Magonjwa yanayoathiri kinga kama vile virusi vya ukimwi na saratani
- Watumiaji wa dawa za kulevya
- Wanawake wajawazito