Home VIWANDAMIUNDOMBINU Soko la kisasa Kisutu kugharimu Bilioni 13

Soko la kisasa Kisutu kugharimu Bilioni 13

0 comment 79 views

Ujenzi wa soko la kisasa la Kisutu unatarajiwa kuanza mwezi ujao na inatarajiwa kuwa, soko hilo jipya mbali na kuwa na uwezo wa kuchukua wafanyabiashara 1,500 pia litakuwa na huduma nyingine muhimu kama vile benki, maegesho ya magari, machinjio na mabucha.

 

Kwa mujibu wa Meya wa Manispaa ya Ilala Charles Kuyeko, Halmashauri ya Ilala imesaini mkataba na kampuni ya ujenzi ya Mohammed na kwamba kiasi cha Sh. 13.48 bilioni zimetolewa na serikali kuu kwa ajili ya ujenzi wa soko hilo la ghorofa nne.

 

Kuyeko ameeleza kuwa ujenzi huo utakamilika ndani ya miezi 18 na utawasaidia wafanyabiashara wa eneo hilo kufanya shughuli zao katika mazingira mazuri hasa katika misimu ya mvua.

 

Takribani wafanyabiashara 633 wa eneo hilo watatakiwa kuhamia eneo la Mkunguni na stendi ya zamani ya Kisutu ili kupisha ujenzi huo. Baadhi ya wafanyabiashara wa eneo hilo wamefurahishwa na ujenzi huo na kusema utawawezesha kujiongezea kipato.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter