• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Anachoweza mwanaume, mwanamke anaweza pia

Patricia Richard by Patricia Richard
June 29, 2018
in WANAWAKE NA MAENDELEO
0
Wanawake washirikishwe zaidi kiuchumi- Balozi Donnell
Share on FacebookShare on Twitter

Kumekuwa na malalamiko kwa muda mrefu sasa kuwa hakuna usawa wa kijinsia nchini. Tatizo hili sio la hapa kwetu pekee bali lipo katika mataifa mengi duniani. Wanawake hawapewi vipaumbele na kuwekwa mstari wa mbele kama ilivyo kwa wanaume katika sekta mbalimbali za maendeleo. Makundi na taasisi mbalimbali zimejitokeza kukemea ubaguzi wa kijinsia lakini bado kuna changamoto kubwa katika kutatua tatizo hili sugu.

Swali la kujiuliza hapa ni, kwanini jamii inafikiria ni sawa kumuweka mwanamke katika ngazi ya chini na kuamini kuwa wanaume ndio watawala? Chimbuko hasa la imani au fikira hii ni nini? Kwanini wanawake hawahusishwi na kushirikishwa katika sekta muhimu za kukuza uchumi sawa na wanaume?

Wanawake hasa wa vijijini wanaachwa nyuma kimaendeleo. Mwezi Mei mwaka jana, Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) lilisema katika moja ya taarifa zake kuwa, inasikitisha na kufadhaisha kuona ukosefu wa usawa wa kijinsia barani Afrika. Shirika hilo lilisisitiza kuwa katika kundi hilo, wanawake ni wengi. Takwimu za Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa idadi ya wanawake wasiojua kusoma na kuandika ipo juu zaidi kulinganisha na ile ya wanaume.

Ni muhimu kujiuliza je hatua gani zinachukuliwa hapa nchini ili kupambana na hali hii? Serikali inatengeneza njia ili kuhakikisha wanawake wana haki sawa kama wanaume? Kisheria, kuna hatua zozote zinazochukuliwa ili kuhakikisha wanaotekeleza vitendo hivi vya kibaguzi wanaadhibiwa? Watoto wetu wanafundishwa kuanzia ngazi ya familia kuwa wanawake na wanaume wote ni sawa? Haya ni baadhi ya maswali muhimu ya kujiuliza.

Takwimu za Jukwaa la Uchumi Duniani zinaonyesha kuwa wanawake wengi hunyimwa nafasi za kazi katika idara mbalimbali japokuwa vyeti vyao huonyesha wana elimu sawa na wanaume. Katika takwimu hizo pia, inaonekana wanawake hupata fursa finyu za kiuchumi na kibiashara huku wanaume wengi wakipata fursa hizi kwa uraisi zaidi.

ADVERTISEMENT

Ni wakati sasa wa wanawake kupigania usawa na kuacha kulalamika bila ya kuchukua hatua zozote. Wanawake wanapaswa kujituma zaidi na kulenga mambo makubwa wawapo katika mahala pao pa kazi. Uonevu huu hautafika mwisho kama wanawake wenyewe hawatakuwa mstari wa mbele kuulaani na kuukemea. Ni wakati wa kuonyesha jamii kuwa wao pia wanaweza na hawatokaa kimya pale ambapo wanaona wanaonewa na kunyimwa haki zao za msingi kwa kisingizio cha kwamba wao sio wanaume.

Serikali nayo ina wajibu wa kuweka mazingira rafiki kwa wanawake. Viongozi wa kike nao watumie sauti waliyonayo kukemea ubaguzi wa kijinsia na pia watumie nguvu yao kuinua wanawake na watoto wa kike kwa ujumla. Changamoto hii ipo kwa kiasi kikubwa hapa nchini lakini wanawake wakiungana na kupiga vita tatizo hili kwa umoja, basi bila shaka watapiga hatua.

 

Tags: maendeleouchumiUNDP
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Mchango mkubwa walionao washauri wa biashara

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In