Home KILIMO Baraza la Chuo cha Taifa cha Sukari lazinduliwa

Baraza la Chuo cha Taifa cha Sukari lazinduliwa

0 comment 155 views

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amezindua Baraza la Chuo cha Taifa cha Sukari na kulitaka Baraza hilo kuhakikisha kuwa inakuwa Kituo cha Umahiri cha kuboresha sekta ya sukari nchini.

Katika uzinduzi huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Wizara ya Kilimo-Dodoma na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Mweli, Bashe amelitaka Baraza hilo kuhakikisha linatanua zaidi utendaji kazi wa chuo kutoka kuwa cha kuwafundisha wanafunzi na kuwa nguzo muhimu ya mabadiliko ya sekta ya sukari.

“Chuo hiki kinatakiwa kuwa Kituo cha Umahiri, kiwe ndio mahala pa kuchangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya kilimo cha miwa.

Nataka kiwe kina uwezo wa kusaidia katika kuongeza thamani ya sukari, kisaidie mbinu za kibunifu kwa kampuni za sukari ili zizalishe sukari ya matumizi ya kawaida na ya viwandani, kisiwe chuo tu kwa ajili ya wanafunzi peke yake” amesema.

Aidha, ameliagiza Baraza hilo kuhakikisha kuwa chuo kinafanya kazi kwa ukaribu na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania(TARI) na wadau wengine katika kilimo kuhakikisha wakulima wadogo na wakubwa wa miwa wanalima kwa tija.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter