Home KILIMOKILIMO BIASHARA Soko la zabibu bado tatizo

Soko la zabibu bado tatizo

0 comment 113 views

Wakulima wa zabibu kutoka kata ya Hombolo, Dodoma wameendelea kuomba serikali kuwatafutia wawekezaji wengine ili wasiendelee kupata hasara kutokana na mazao yao kuharibika kwa kukosa soko. Wakulima hao wamesema hayo kwa Mkuu wa mkoa huo Dk. Binilith Mahenge alipotembelea mashamba hayo na kujionea uharibifu huo unaoendelea. Wakulima hao wamesema ili hali hiyo isiendelee kutokea inatakiwa kuongeza viwanda kwani wanazalisha kwa wingi.

“Tangu serikali ya awamu ya tano iseme tufanye kazi, zabibu zinazotoka nchini ni zaidi ya hizi mnazozishuhudia sasa, zaidi ya miaka mitatu tutatengeneza bomu la hatari la kukosa soko hapa”. Amesema mmoja wa wakulima hao.

Wakulima hao wameomba serikali kuangalia uwezekano wa kuleta wawekezaji zaidi katika eneo la Hombolo wakidai aliyekuwepo hivi sasa (kiwanda cha Cetawico) ana uwezo mdogo wa kununua zabibu hizo.

Baada ya kujionea hali halisi, Dk. Mahenge ametoa maagizo kwa Katibu Tawala wa mkoa huo kuwaita awekezaji wote wa viwanda pamoja na wanunuaji zabibu ili wapate nafasi ya kujadiliana na kuangalia uwezekano wa kutatua tatizo hilo.

“Pia ni vyema mkaanzisha chama cha ushirika wa zabibu kama ilivyo kwenye mazao mengine kwa kuwa mkakati uliopo ni kuinua zao hilo liwe kama mazao mengine ikiwemo kahawa”. Ameshauri Mkuu hyo wa mkoa.

 

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter