Home BENKI Kijani Bond kutoa Riba ya 10.25%

Kijani Bond kutoa Riba ya 10.25%

0 comment 101 views

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo amezindua uuzaji wa hatifungani ya kijani “Kijani Bond” ya benki ya CRDB yenye riba ya 10.25%.

Taarifa ya CRDB inasema Kijani Bond inatoa fursa kwa watu wote kuwekeza kuanzia Sh. laki 5 kwa riba ya asilimia 10.25 kwa mwaka.

“Katika hatua hii ya mwanzo benki inatarajia kukusanya Sh. bilioni 55 zitakazoelekezwa kufadhili miradi inayotunza mazingira na kuzingatia mabadiliko yaa tabianchi,” imesema taarifa hiyo.

Kijani Bond ni hatifungani ya kwanza ya kijani Tanzania , na ya kwanza kwa ukubwa kusini mwa Jangwa la Sahara.

Hatifungani hiy, inatoa fursa ya uwekezaji kwa muda wa miaka 5 ikiwa na thamani ya dola za Marekani milioni 300 sawa na Sh. bilioni 780.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter