Home BIASHARAUWEKEZAJI Rais Samia akaribisha wawekezaji wa India

Rais Samia akaribisha wawekezaji wa India

0 comment 131 views

Rais Samia Suluhu Hassan amewakaribisha wawekezaji wa India kuja kuwekeza Tanzania akiahidi mazingira rafiki ya biashara na maendeleo ya uchumi.

Mkuu huyo wa nchi, ameyasema hayo New Delhi wakati akizungumza na wawekezaji katika jukwaa la biashara na uwekezaji la Tanzania-India katika ziara yake ya siku tatu nchini India.

Rais Samia amesema Tanzania inatekeleza maendeleo na mageuzi ya uchumi ya Afrika yanayochochewa na sekta binafsi na uwekezaji katika kukuza uchumi.

“Kama sehemu ya mageuzi hayo, Tanzania tunatumia teknolojia ambayo inawawezesha wawekezaji kutoka nje ya nchi kuweza kusajili biashara zao kwa njia ya mtandao kabla ya kufika nchini,” ameeleza Rais Samia.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter