Home Lifestyle Wafanyakazi wa Benki ya Dunia wafanya usafi wa fukwe jijini Dar es Salaam

Wafanyakazi wa Benki ya Dunia wafanya usafi wa fukwe jijini Dar es Salaam

0 comment 140 views

Leo, wafanyakazi wa  Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania  wakiongozwa na Mkurugenzi wao, Bi. Bella Bird, wamefanya  usafi kwenye fukwe za bahari eneo la Coco Beach jijini Dar Es Salaam.

Usafi huo ulifanyika kama jitahidi za Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira.

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia (WB) nchini, Bella Bird (kushoto) akiwa amejumuika na baadhi ya wafanyakazi wa Benki hiyo baada ya kuhitimisha zoezi lililofanyika katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam

“Ujumbe wetu kwa jamii ni wawe na wajibu wa kuepuka uchafuzi,  kuondoa utamaduni wa kutupa taka ovyo na kua na tabia ya kuchakata. Tumefurahi Serikali imechukua hatua kubwa kuzuia matumizi ya mifuko ya plastiki na tunatumaini wataendelea kudhibiti”,alisema Bi.Bird.

Aliendelea kusema kwamba upunguaji wa taka za mifuko ya plastiki hakika ni kitu kikubwa kwa Tanzania kusherehekea. Pia alisema hatua itayofuata ni kupiga marufuku mirija ya vinywaji kwa kua haina matumizi yoyote muhimu kwa karne hii.

Pichani juu na chini ni Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania wakionyesha taka za plastiki ikiwemo miraji na mifuko ya lambalamba bidhaa za Ukwaju zinazotengenezwa na kampuni ya Azam iliyokuwa imetapakaa katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.

Nao wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania walisema kila mmoja ana jukumu la kutunza mazingira.

“Wote tunajukumu kwenye  hizi taka. Makampuni ya vyakula na vinywaji  yashiriki kutoa elimu kwa jamii, kupanga usafi, kuweka pipa za taka na kusaidia uzoaji taka kama jukumu la kampuni kwa jamii”,walisema wafanyakazi hao.

Nae, Carlos Mdemu ambaye ni mratibu wa  ‘Nipe Fagio’ alisema “kuweka pipa za taka maeneo ya fukwe na mtaani ni mpango mzuri, lakini kwenye baadhi ya maeneo tumeona mapipa yanajaa na hakuna  anayekuja kuyazoa, kwahiyo watu wanabidi wajue majukumu yao pia”.

Mdemu aliendelea kusema “kuwatoza faini  kwa kutupa taka ovyo inafanywa na Manispaa ya Ilala na ni nzuri. Lakini kuongeza ufahamu inaweza kua muhimu zaidi ili kwamba watu wengi wakiwa wanajua, unapunguza nguvu ya kuwatoza faini”.

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia (WB) nchini, Bella Bird (wa pili kulia) akipata maelezo kutoka kwa Carlos Mdemu (wa tatu kushoto) ambaye ni Mratibu wa Nipe Fagio baada ya kuhitimisha zoezi hilo lililofanyika katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach wafanyakazi hao walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.Pichani walioinama chini ni vijana wa Nipe Fagio wakijaribu kufanya tathmini ni taka gani zaidi zimejitokeza kwa wingi wakati wa zoezi la usafi katika fukwe hizo.

Kuhusiana na taka za plastiki Mdeme alisema “kwa sasa, taka yenye changamoto tuliyoona ni chupa za plastiki zenye rangi na vifungashio vya chakula (aiskrimu n.k).  Chupa za plastiki za rangi hazikusanywi kwa ajili ya kuchakata kwasababu hazina soko kwa  wakusanyaji”.

Pichani juu na chini ni Baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania wakionyesha taka za plastiki ikiwemo miraji na mifuko ya lambalamba bidhaa za Ukwaju zinazotengenezwa na kampuni ya Azam iliyokuwa imetapakaa katika eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.

“Hapo nyuma tulipofanya usafi wa fukwe, tuligundua hesabu za taka za mifuko ya plastiki ni zaidi ya asilimia 50. Hii imebadilika, leo tumekusanya si zaidi ya asilimia 10” alisema Carlos Mdemu.

Sehemu ya wafanyakazi wa Benki ya Dunia ofisi ya Tanzania wakirejea na mifuko iliyosheheni taka za plasitiki baada ya kuhitimisha zoezi hilo eneo la fukwe za bahari ya Coco Beach walipojitolea kusafisha fukwe hiyo ikiwa ni juhudi za kuunga mkono mpango wa serikali kudhibiti matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo ilikua ni chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira jijini Dar es Salaam.

Wakihitimisha usafi katika fukwe za Coco Beach wafanyakazi hao walisema “tumeacha alama ndogo ukilinganisha na kinachotakiwa kufanywa. Lakini hii ndiyo sababu kwanini tumefanya na kwanini wote inabidi tuunganishe mikono na kuacha alama kubwa zaidi.

“Tunatekeleza tunachokisema, Benki ya Dunia Tanzania tunasema hapana kwa plastiki, weka fukwe na bahari yetu safi, sema hapana kwa matumizi ya plastiki, saidia mapambano dhidi uchafuzi wa plastiki” walisema wafanyakazi hao.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter