• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Monday, January 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Mbegu za maboga ni fursa mpya mjini

Dennis Msotwa by Dennis Msotwa
August 18, 2018
in UJASIRIAMALI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Siku za hivi karibuni imeshuhudiwa biashara mpya ikiibuka mjini huku watu waliopo vijijini wakiwa bado hawajaigundua fursa hii ya kiuchumi hasa katika shughuli za kilimo.

Nikiwa maeneo ya makumbusho naamua kuingia supermarket moja mpya iliyojengwa hivi karibuni. Moja ya vitu vinavyonishangaza ndani ya supermarket hiyo ni kukutana na bidhaa ya mbegu za maboga.

Ni kitu ambacho sikutegemea kukutana nacho katika maeneo hayo ukizingatia supermarket ni moja ya sehemu ambayo huuzwa vitu ghali na vyenye kupendeza. Nilipojaribu kuuliza bei nikaambiwa pakiti moja inauzwa Tsh. 1000.

Kwa jamii nyingi za Tanzania biashara hii ni mpya kabisa kwa sababu walio wengi wamekuwa wakiitupa bidhaa hiyo huku wakiamini kitu cha muhimu katika zao hilo ni maboga na majani yake ambayo ni mboga.

ADVERTISEMENT

Hii ni fursa mpya ya kiuchumi ambayo lazima itiliwe mkazo ukizingatia ukweli kwamba biashara hii imekuwa ikikua kwa kasi.

Pesatu.com imejaribu kuwauliza wakazi wa Nyanda za juu kusini ikiwa ni moja kati ya jamii zinazolima zao hili katika mikoa ya Mbeya, Songwe na Rukwa ambao wengi wamekiri mbegu za Maboga zimekuwa zikiuzwa 4000 hadi 6000 kwa sado hasa maeneo ya vijijini huku wakazi wengi wa maeneo hayo wakiwa bado hawachukulii mbegu za maboga kama fursa ya kiuchumi.

Soko la Kisutu lililopo maeneo ya Posta Jijini Dar Es Salaam ni moja kati ya masoko maarufu hapa jijini kwa uuzaji wa vyakula na mazao, ikiwemo, matunda, mboga za majani na nafaka, Pesatu.com iliweka kambi mwishoni mwa wiki hii na kufanya mahojiano na Bwana Saleh Abdul mmoja kati ya wauza nafaka waliopo katika soko hilo ambaye alikiri wazi kuwa bidhaa hiyo imekuwa ikipanda bei kila siku huku nusu kilo ya Mbegu hizo ikiuzwa kwa Tsh. 4000 sawa na 8000 kwa kilo.

Hata hivyo inashauriwa kuwa mkulima wa zao hili ni ni vema akafuata ushauri wa kitaalamu hasa juu ya mbegu bora yenye kuzalisha mbegu nyingi za maboga.

Kwanini bidhaa hii imekuwa kwa kasi kiasi cha kuuzwa Supermarket?

Bidhaa hii inakua kila iitwapo leo kutokana na kazi kubwa za mbegu hizo katika mwili wa binadamu ikiwa ni pamoja na kuzuia ugonjwa wa kisukari,mbegu hizi zina kiasi kikubwa cha madini ya Zinc yanayosaidia kuimarisha kibofu cha mkojo,Kinga ya Saratani ambapo Imethibitika kwamba watu ambao hula mlo wenye kiasi kingi cha mbegu za maboga wamegundulika kuwa na hatari ndogo sana ya kupatwa na saratani za tumbo, matiti, mapafu na kibofu, dawa ya uvimbe ikithibitishwa na tafiti kadhaa ambazo zimeonesha kuwa mbegu za maboga zina mafuta yenye uwezo wa kutoa kinga dhidi ya magonjwa ya uvimbe (inflamatory diseases) sawa na dawa aina ya Indomethacin, lakini mbegu hizi hazina madhara kama ilivyo kwa hiyo dawa.

Nini kifanyike ili kuhakikisha uzalishaji wa kutosha wa zao hili?

Wazalishai wengi wa zao hili wanapatikana maeneo ya vijijini na bado hawachukulii suala hili kama fursa ya kiuchumi, hivyo elimu ya kutosha lazima itolewe ili kuhakikisha kunakuwepo na uzalishaji wa kutosha na upatikanaji wa uhakika wa bidhaa hii sokoni kwa kuwaelimisha wakulima wa maboga kuichukulia kama fursa mpya ya kiuchumi.

Kupanga bei moja na inayoeleweka katika soko,Ukiangalia kwa makini hakuna uwiano kati ya bei za wazalishaji na bei katika soko. Wakulima wanauza sado moja kwa Tsh 4000 hadi 6000 huku wafanyabiashara wakiuza nusu kilo kwa Tsh. 4000

 

 

Tags: biasharafursamabogamagonjwambeguuchumi
Dennis Msotwa

Dennis Msotwa

Next Post

Wafanyabiashara mipakani watakiwa kuchangamkia fursa

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In