Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi Vodacom ikishirikiana na Taasisi ya usimamizi wa miradi (PMI) zimeshiriki katika mazungumzo ya uchumi wa kidijitali na kuainisha fursa mbalimbali zitokanazo na uchumi huo.
Chini ni baadhi ya picha katika mazungumzo hayo.

Kaimu Mkurugenzi wa kampuni ya Vodacom Tanzania, Bw Hisham Hendi akitoa mada kuhusiana na uchumi wa kidijitali kaatika mkutano wa mwaka wa Taasisi ya Usimamizi wa Miradi uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Universal Communication Service Access Fund (UCSAF), Peter Ulanga akizungumza katika mkutano wa mwaka wa Taasisi ya Usimamizi wa Miradi (PMI) uliofanyika jijini Dar es Salaam mapema jana. Mkutano huu umelenga kujadili ukuaji wa uchumi wa kidijitali.

wa Taasisi ya Usimamizi wa Miradi (PMI, Bw Anael Ndosa, akichangia mada kuhusiana na uchumi wa kidijitali kaatika mkutano wa mwaka wa Taasisi ya Usimamizi wa Miradi uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi wa kampuni ya Vodacom Tanzania, Bw Hisham Hendi akichangia mada kuhusiana na uchumi wa kidijitali kaatika mkutano wa mwaka wa Taasisi ya Usimamizi wa Miradi uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Universal Communication Service Access Fund (UCSAF), Peter Ulanga.