Home BIASHARA Vivutio vya utalii Tanzania vyavutia Hispania

Vivutio vya utalii Tanzania vyavutia Hispania

0 comment 62 views
Katika Maonesho ya Utalii ya FITUR yanayoendelea nchini Hispania, vivutio vya utalii vinavyopatikana nchini  vimewavutia washiriki wengi.
Kaimu Meneja wa Mikutano na Matukio wa Bodi ya Utalii (TTB) inayoratibu maonesho hayo kwa upande wa Tanzania Bi. Lily Fungamtama amesema kuwa wamepokea mawakala wengi wa utalii walioonyesha kuvutiwa na vivutio hivyo na kuweka miadi ya kuvitembelea katika siku za usoni.
Hispania ni miongoni mwa masoko makubwa yanayoleta watalii nchini ikiwa inashika nafasi ya 11 kwa kuleta watalii Tanzania.
Maonesho hayo yanatarajiwa kufanyika kwa siku tano.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter