• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Wednesday, June 29, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Wajasiriamali wa kati wameongezeka kwa kiasi kikubwa nchini

Jinsi Sahara Ventures inavyounganisha wawekezaji wazawa na makampuni ya nje ya uwekezaji

Pesatu Reporter by Pesatu Reporter
November 16, 2020
in BIASHARA, UWEKEZAJI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Jumanne Rajabu Mtambalike ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Sahara Ventures inayojishughulisha na kuunganisha wajasiriamali wa kati na makampuni ya uwekezaji nje ya nchi kidigitali.

Kampuni hiyo ambayo ilianzishwa mwaka 2016, ni atamizi ya kusaidia makampuni madogo madogo kuwa tayari kukutana na wawekezaji mbalimbali kwa kuwapa ubunifu, ushauri na teknolojia.

Mtambalike ambae pia ni mjasiriamali wa kati kwa kutumia mitandao, anasema tangu kuanzishwa kwa Sahara Ventures wameweza kufikia makampuni takribani 2000 kupitia tamasha la Sahara Spark ambalo hukusanya watu kutoka Tanzania na nchi mbalimbali barani Afrika.

Tamasha hili, hufanyika kila mwaka likiwa na lengo la kukusanya wajasiriamali pamoja na vijana kuwajengea uwezo katika sekta mbalimbali za uwekezaji ikiwemo kilimo, fedha pamoja na afya.

Mtambalike anaeleza kuwa wajasiriamali wa kati wameweza kuongezeka kwa asilimia kubwa kutokana na kukua kwa teknolojia pamoja na fursa mbalimbali zilizopo ikiwemo matamasha ambayo yanawapa fursa ya kueleza biashara zao na maonyesho.

Anasema teknolojia pia inachangia sana kuongozeka kwa wajasiriamali kutokana na matumizi ya masoko ya kidigitali (Digital Marketing).

ADVERTISEMENT

Anasema kupitia masoko hayo ya kidigitali wanaweza kuunganisha wajasiriamali wa kati na wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali.

“Tunafanya kazi kwa njia ya mtandao ambapo tunawasaidia wajasiriamali ambao tayari wana biashara zinazoendelea kuwaunganisha na wawekezaji katika sekta husika. Hii imeleta mafanikio makubwa sana, imesaidia makampuni madogo kukua na kuongeza uwekezaji kwa kiwango kikubwa,” amesema Mtambalike.

Akizungumzia swala biashara ya mitandao Mtambalike amesema kwa jinsi teknolojia inavyokuwa kwa kasi ndivyo wafanyabiashara wengi wanavyotumia mitandao kukuza biashara.

“Biashara nyingi sasa zimehamia mitandaoni kutokana na kukua kwa teknolojia, na huku sasa ndipo kwenye fursa nyingi zaidi. Niwape wito vijana kujifunza jinsi ya kutumia mitandao hii kujipatia kipato kuliko kutumia mitandao kwenye mambo yasiyo na maana,” amesema Mtambalike.

Ameeleza pia kuwa wanashirikiana na taasisi mbalimbali ikiwemo Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) katika kuwajengea uwezo vijana katika kazi za ubunifu na ujasiriamali.

Pesatu Reporter

Pesatu Reporter

Next Post

NMB yaja na ATM kubadili fedha za kigeni

Discussion about this post

Habari Mpya

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 28, 2022

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 28, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 28, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 28, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 28, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 28, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

by Jensen Kato
June 28, 2022
0

Kilimo biashara kinaendelea kukua barani Afrika na muda umefika kwa watu hususani vijana kuchagamkia fursa mbalimbali zinazotokana na kilimo. Watu...

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 28, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In