Home WANAWAKE NA MAENDELEO Rais Mwinyi: Tutaweka mkazo uzalishaji mwani Zanzibar

Rais Mwinyi: Tutaweka mkazo uzalishaji mwani Zanzibar

0 comment 58 views

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali yake inakusudia kuweka mkazo zaidi kwenye sekta ya mwani ili kuzalisha bidhaa zenye ubora na kuzipatia soko la uhakika.

Dk. Mwinyi ameyasema hayo Agosti 21, 2024, Ikulu Zanzibar wakati akizungumza na Balozi wa Umoja wa Ulaya Tanzania Christine Grau.

Amesema asilimia 99 ya wakulima wa zao la mwani Zanzibar ni wanawake, hivyo amemueleza balozi huyo kuangalia haja ya kuwaunga mkono wanawake na wakulima wa mwani nchini, hasa kwa mafunzo na vifaa vya kisasa ili wazalishe mwani wenye ubora utakaoendana sambamba na soko la uhakika.

Mbali na mambo mengine ya maendeleo na uwekezaji ikiwemo utalii, Rais Dk. Mwinyi pia amemueleza Balozi Grau kuwa Uchumi wa Buluu ni sera kuu ya uchumi wa Zanzibar, hivyo amemueleza kuangalia fursa zinazotokana na sera hiyo.

Kwa upande wake, Balozi Christine Grau amesifu juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inayoongozwa na Rais Dk. Mwinyi na kueleza kuwa wanafanya kazi kwenye maeneo mbalimbali, ikiwemo kushirikiana na jamii kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo na ustawi wa jamii Unguja na Pemba.

Balozi wa Umoja wa Ulaya Tanzania Christine Grau.

Soma: Tanzania ya kwanza kilimo cha mwani Afrika

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter