Home BENKI CRDB yapata kibali Hatifungani ya Kijani

CRDB yapata kibali Hatifungani ya Kijani

0 comment 83 views

Benki ya CRDB imekabidhiwa kibali cha kuuza Hatifungani ya Kijani “Kijani Bondi” ya miaka 5 yenye thamani ya dola za marekani Milioni 300 sawa na Sh. Bilioni 780 na Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).

Kibali hicho cha kutoa hatifungani ya kijani kimekabidhiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa CMSA, Nicodemus Mkama kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela aliyeambatana na Mwenyekiti wa Bodi, Dkt. Ally Laay katika hafla iliyofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam Agosti 24, 2023.

Kibali hicho kinaifanya Benki ya CRDB kuwa ya kwanza nchini kutoa hatifungani ya kijani, na ya kwanza kwa ukubwa Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Taarifa ya CRDB inasema Kijani Bond itarahisisha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kufadhili miradi rafiki kwa mazingira na kuchochea ufikiaji wa Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDG).

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter