Home KILIMOKILIMO BIASHARA Waziri Mkuu azindua migahawa ya kahawa inayotembea

Waziri Mkuu azindua migahawa ya kahawa inayotembea

0 comment 68 views

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Kassim Majaliwa amezindua Migahawa ya Kahawa inayotembea ikiwa ni mkakati wa kuongeza ushiriki wa vijana katika mnyororo wa thamani wa Tasnia ya Kahawa nchini.
Majaliwa amezindua migahawa hiyo Agosti 1, 2024 baada ya kufungua Maonesho ya Kilimo ya Kimataifa ya Nane Nane 2024 yanayofanyika Kitaifa kwenye Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.

Waziri Mkuu ametoa pongezi kwa Wizara ya Kilimo pamoja na Bodi ya Kahawa kwa kufanya ubunifu wa mradi huo ambao utakuwa chachu ya ongezeko la ajira nchini hususan kwa vijana.

Migahawa hiyo ya Kahawa inayotembea, itasimamiwa na Bodi ya Kahawa Tanzania kupitia Mradi wa Jenga Kesho iliyo bora (BBT) ambao upo chini ya Wizara ya Kilimo.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mgahawa wa kahawa unaotembea.

About Us

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905.

Editors' Picks

Newsletter