• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, June 26, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Tukuze vipaji, ni ajira

Patricia Richard by Patricia Richard
May 16, 2018
in BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Mara nyingi watu wengi hutegemea tu elimu kuwa ndio mkombozi pekee katika maisha. Ni kweli kuwa huwezi kufika mbali na kuendelea bila ya kuwa na elimu. Lakini umeshawahi kufikiria kuhusu kipaji ulichonacho? Kuendeleza kipaji chako sio njia moja wapo ya kujiajiri au kuajiriwa? Ni watu wangapi hapa nchini hupata fursa ya kukuza vipaji vyao na kujiendeleza kiuchumi?

Katika jamii zetu, wazazi wengi huwa hawaangalii sana vipaji vya watoto wao. Wengi huona kama sio kitu ambacho kinampatia mtu fursa na kumjengea ajira rasmi. Wazazi wengi hupambana watoto wao wapate elimu na kufanya hivyo wakati wengine kunaua kipaji ambavyo kama vingeendelezwa, vingeweza kuwa chanzo cha ajira na kipato kizuri tu. Mifumo yetu ya elimu nayo haijaweka mkazo wa kutosha katika kukuza vipaji vya wanafunzi na kuwafungulia milango ili waone kuwa navyo pia vinaweza kuwa ajira yao.

Ni muhimu kujiuliza kuwa kwanini watu wengi huona kama kukuza kipaji cha mtoto sio jambo jema? Kwani hakuna mifano hai ya watu ambao waliamini katika vipaji vyao na wakaendelea? Ni kwanini asilimia kubwa ya wazazi huona kama sanaa ni uhuni na si ajira rasmi kama zilivyo ajira nyingine? Watoto wenye vipaji waviache tu vipotee bila kuvitumia?

ADVERTISEMENT

Ni dhahiri kuwa lazima hatua zichukuliwe ili kuondokana na dhana ya kwamba maendeleo hayawezi kupatikana kutokana na kipaji cha mtu. Kama wazazi ama walezi wote wangefikiria hivyo basi kusingekuwa na wachoraji, wachongaji vinyago, waigizaji na hata wanamuziki kote hapa nchini. Sanaa ni sekta muhimu katika maendeleo kama zilivyo hizo nyingine lakini mara nyingi huwa haipewi kipaumbele.

Kupitia shughuli za kisanaa kama vile muziki, uigizaji na hata uchoraji watu wameweza kujiajiri na wengine wameenda mbali zaidi hadi kufungua makampuni yao binafsi na kutoa ajira kwa wengine. Hakuna anayekataa kuwa elimu ni ufunguo wa maisha na ni muhimu kusoma na kufikia malengo yako lakini wakati unafanya hivyo, kama una kipaji na unaamini unaweza kufika nacho mbali ni vizuri kukiendeleza na kuona ni wapi kitakupeleka.

Vijana nao wanatakiwa kujiamini kutumia vipaji vyao kujiajiri na kuanzisha miradi mbalimbali ya ujasiriamali ili kupiga vita tatizo la ajira lililopo kote hapa nchini. Kwa kujiajiri na kuweza kujiiingizia kipato, pia wanapata nafasi ya kuchangia katika pato la taifa. Ni muhimu kuonyesha juhudi na nia ya kufanikiwa ili hata wale ambao hawakuwa na imani kuwa vipaji vinaweza kutumika kujiajiri waone kuwa inawezekana.

Tags: ajiraelimumaendeleoSanaaujasiriamaliVipaji
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Dangote kutumia gesi asilia

Discussion about this post

Habari Mpya

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 24, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 23, 2022

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 23, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 22, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 22, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 20, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 24, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

by Pesatu Reporter
June 23, 2022
0

Mapendekezo yamepitishwa kwa kila Mtanzania kuwa na bima ya afya. Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM (NEC) leo 23...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In