• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Wednesday, June 29, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Benki ya NMB kuvutia watalii kutoka barani Asia kupitia UnionPay

Benki ya NMB yaingia ubia na Union pay International, yazindua jukwaa la biashara mtandaoni

Pesatu Reporter by Pesatu Reporter
October 10, 2020
in BIASHARA
0
Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar – Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akiashiria utoaji fedha kwa kutumia kadi ya Union Pay katika ATM ya NMB wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo visiwani Zanzibar. Wanaoshuhudia ni viongozi wa juu wa benki ya NMB wakiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu Ruth Zaipuna (wapili kushoto). Picha na Mtandao NMB

Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar – Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akiashiria utoaji fedha kwa kutumia kadi ya Union Pay katika ATM ya NMB wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo visiwani Zanzibar. Wanaoshuhudia ni viongozi wa juu wa benki ya NMB wakiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu Ruth Zaipuna (wapili kushoto). Picha na Mtandao NMB

Share on FacebookShare on Twitter

Katika kuwavutia watalii kutoka barani Asia na kwingineko duniani, benki ya NMB imeshirikiana na kampuni ya kimataifa ya kadi –Union Pay International (UPI) ili kuwawezesha watumiaji wa kadi za UnionPay kufanya miamala kwenye mashine za kutolea fedha (ATM) na PoS za benki hiyo.

NMB pia imezindua jukwaa la biashara ya mtandaoni ‘E- Commence platform’  litakalowezesha wafanyabiashara kufanya miamala kupitia tovuti zao.

ADVERTISEMENT

‘E Commence platform’ itawawezesha wafanya biashara na makampuni ya huduma kupokea malipo kimtandao kupitia tovuti zao, bila wateja kutembelea sehemu za biashara zao.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB Ruth Zaipuna amesema ushirikiano na UPI utaleta unafuu na uharaka wa kufanya miamala kwa watumiaji wa kadi za UPI watakao kuwa wanapata huduma kwenye  ATM na PoS za NMB muda wote.

Zaipuna amesema “hii ni hatua muhimu sana katika kuleta huduma bora kwa wateja wetu, ni fursa kwa wafanya biashara hususani sekta ya utalii, hoteli, na maduka katika kuwezesha biashara za kimataifa kupitia malipo mtandao yanayowezeshwa na benki ya NMB,”.

Amefafanua kuwa  “Kwa mtandao wetu wa zaidi ya PoS 1,750 na ATM Zaidi ya 800 nchini, huduma hii inategemewa kuleta mapinduzi kwa watumiaji wa kadi za UnionPay.

Kadi hizi  zinajulikana kama nyenzo muhimu ya malipo kwa kufanikisha biashara, utalii na muingiliano wa kiutamaduni kati ya bara la Afrika na Asia. Ushirikiano huu kati ya benki ya NMB na UnionPay International utaongeza matumizi ya kadi za UnionPay nchini na katika miamala ya kimataifa na inaashiria mapinduzi ya teknolojia ya malipo kupitia kadi”

Meneja Mkuu wa UnionPay International tawi la Afrika – Luping Zhang amesema wanayo furaha kushirikiana na benki ya NMB kuleta huduma hii muhimu kwa sekta ya utalii Tanzania.

Hang amesema UPI ina takribani kadi bilioni 8.4 zilizopo katika nchi 61 duniani na inajivunia kuwa kampuni kubwa zaidi ya kadi duniani.

Kadi hizi za Union Pay zitasaidia kuongeza wigo wa mauzo na malipo ya watalii nchini, kwani kabla ya hapo malipo mengi yalifanyika nje ya nchi na hivyo kulikosesha taifa mapato yatokanayo na biashara ya utalii.

Kwa bara la Afrika, ipo katika nchi 50.

 

Pesatu Reporter

Pesatu Reporter

Next Post
Balozi wa Uholanzi nchini Tanzania Jeroen Verheul pamoja na Mkurugenzi mtendaji wa TSA Zahoro Muhaji baada ya utiaji saini mkataba wa kuboresha na kuendeleza ujasiriamali.

Tanzania na ubalozi wa uholanzi wasaini mkataba wa kuboresha na kuendeleza ujasiriamali

Discussion about this post

Habari Mpya

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 28, 2022

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 28, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 28, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 28, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 28, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 28, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

by Jensen Kato
June 28, 2022
0

Kilimo biashara kinaendelea kukua barani Afrika na muda umefika kwa watu hususani vijana kuchagamkia fursa mbalimbali zinazotokana na kilimo. Watu...

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 28, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In