• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, January 29, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Huduma za kifedha kupitia simu za mkononi zinachochea kukua kwa mfumo rasmi wa kifedha nchini Tanzania

Athanas Lupatu by Athanas Lupatu
October 8, 2018
in BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Kuimarika kwa mfumo rasmi wa kifedha ni moja ya nguzo katika maendeleo ya jamii yoyote au nchi, na suala hili limeweza kufanyika nchini Tanzania.Labda kwanza tufahamu maana ya neno mfumo rasmi wa fedha? Kulingana na Benki ya Dunia, kuingizwa katika mfumo rasmi wa kifedha, ina maana kwamba watu na wafanyabiashara wanapata huduma  za kifedha zinazofaa na za gharama nafuu  kulingana na matakwa yao, mfano wa huduma hizo ni kama vile kufanya mihamala ya malipo mbalimbali,kuweka akiba,kupata mikopo na huduma za bima.Huduma hizi kwa kipindi kirefu nyuma wamekuwa wakizipata watu wenye akaunti za benki ambazo ziko katika majina yao binafsi zinazoonyesha pia jina la taasisi ya fedha ambazo wanazo akaunti zao.

Mfumo rasmi wa kifedha hupimwa kutokana na asilimia ya watu wazima (waliofikisha umri wa miaka 15), ambao angalau wana akaunti moja kwa majina yao binafsi katika taasisi inayotoa huduma za kifedha ambayo inaendeshwa kwa kufuata kanuni za usimamizi za serikali.

Mfumo huu huwezesha wenye akaunti binafsi kwenye taasisi za kifedha kuweza kupata huduma mbalimbali za kifedha ikiwemo-kujiwekea akiba, kupata mkopo, kutuma fedha, huduma za bima na uwekezaji. Taasisi za kifedha zinazotamblika kutoa huduma za kifedha nchini ni pamoja na mabenki, watoa huduma za fedha kupitia mitandao ya simu kama vile M-PESA ya Vodacom Tanzania, taasisi nyinginezo zilizosajiliwa kutoa huduma hiyo ambazo sio mabenki na vyama vya ushirika.

Mnamo mwaka wa 2017, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Tanzania (BOT) iliona umuhimu wa kuchochea mabadiliko ya wananchi wengi kuingia kwenye mfumo rasmi wa kifedha kupitia utekelezaji wa Mwongozo wa Taifa wa Kuwezesha Wananchi wengi kuwa kwenye mfumo rasmi wa kupata huduma za kifedha wa (NFIF) 2014-2016, ambao ulifanikisha kuboresha sheria za kifedha zilizokuwepo na mpya sambamba na kuanzishwa kwa ushirikiano katika miradi baina ya serikali na sekta binafsi.

Hatua hizi zilisababisha uwekezaji mkubwa mojawapo ikiwa katika sekta ya mawasiliano ambapo makampuni ya simu za mkononi yaliwekeza nchini Tanzania.Uwekezaji huo sasa umefanikisha kwa kiasi kikubwa watu wengi kuingia kwenye mfumo rasmi wa fedha kupitia huduma zinazotolewa kupitia mitandao ya simu za mkononi.

ADVERTISEMENT

Kwa kusimamia na kuhakikisha sheria zinatekelezwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ilichukua hatua nzuri. Kulingana na takwimu, asilimia 74% ya wakazi waliishi ndani ya umbali wa kilometa 5 kufikia sehemu za kupata huduma wanazohitaji mwaka 2017. Pia, 56% ya kundi la watu wazima nchini Tanzania, walikuwa kwenye mfumo rasmi wa fedha kupitia akaunti zao walizokuwa wamefungua kwenye taasisi ya kifedha zilizowawezesha kupata huduma za kifedha kupitia akaunti zao.

Kuwepo kwa idadi ya asilimia kubwa ya wananchi katika mfumo rasmi wa kifedha ulichangiwa na kuanzishwa kwa huduma za kifedha kupitia simu za mkononi, Asilimia 55% ya watu wazima walikuwa na akaunti za fedha za simu, ambapo asilimia 9% walikuwa na akaunti wenye benki tofauti tofauti za benki. Huduma za kifedha kupitia huduma za simu za mkononi zimekubaliwa na wananchi wengi kutokana na urahisi na upatikanaji wake.

Hata hivyo, kuna suala jingine kwenye safari ya kuingizwa watu wengi zaidi katika mfumo rasmi wa kifedha nchini Tanzania, ambalo linahitajiwa kufanyiwa kazi nalo ni kutozingatia usawa wa kijinsia.Upatikanaji wa huduma za kifedha kwenye taasisi zilizokuwa zinatoa huduma hizo miaka ya nyuma zilitumia sheria ambazo zilikuwa hazitoa nafasi kwa wanawake kupata huduma za kifedha kwa urahisi hasa maeneo ya vijijini.Wanawake walichukuliwa kama watu wa kukaa nyumbani na kutunza familia  na kazi ya kutafuta pesa ilikuwa nu jukumu la wanaume pekee.Majukumu ya kifamilia yaliwafanya wanawake kutopata nafasi ya kwenda kwenye mabenki kutafuta njia za kupata huduma za kifedha.

Mfumo rasmi wa kifedha ambao umekuwepo siku nyingi wa kupata huduma za kifedha kwenye mabenki kihistoria umekuwa ukipendelea Wanaume. Kutokana na majukumu ya wanawake ilikuwa ni vigumu kupata huduma za kibenki, hata ambao wangepata nafasi ya kwenda kwenye mabenki kumekuwepo na vikwazo mbalimbali kwao kama vile kuwa na kitambulisho au nyaraka za udhamini kuweza kupata huduma mbalimbali zitolewazo na mabenki.

Tangu mwaka 2008, ilipoanzishwa  huduma ya M-PESA ya Vodacom, huduma za  kifedha kupitia simu ya mkononi  zimeongezeka kwa kasi na kiasi kikubwa nchini hadi kufikia hatua ya  kutumiwa katika huduma zilizokuwa zikitolewa na mabenki.Baadhi ya huduma hizo ni kama vile  kufanya mihamala kwa kushirikiana na mabenki kupitia simu za mkononi ,kuweka akiba na ,mikopo midogo midogo.Huduma hii imekuwa mkombozi kwa wanawake wengi nchini Tanzania ambapo imewawezesha kupata mitaji ya kuendesha biashara zao  ambazo nyingi haziko  katika mfumo rasmi.

Kupitia matumizi ya huduma za kifedha kupitia simu za mkononi, yamewezesha wanawake kufanya shughuli zao kwa ushirikiano mkubwa tofauti na ilivyokuwa hapo awali. Mifumo hii imewezesha makundi ya wanawake kuweza kujiwekea akiba na kupata mikopo ya kuendeleza shughuli zao, pia wemeweza kuanzisha vikundi mbalimbali vya uzalishaji na wengi wao kuendelea kunufaika nchini kote.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inaweza kujivunia kwa kuanzisha sheria na usimamizi ambazo zimefanikisha watanzania wengi kuwa katika mfumo rasmi wa kifedha hasa kupitia huduma za simu za mkononi ambazo zimefanikisha suala hili haraka na kuwafikia wananchi nchini kote.

Kama nchi tumefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa kuleta mapinduzi ya kuwawezesha wananchi wengi kuingia katika mfumo rasmi wa kifedha. Mchango mkubwa wa kuleta mapinduzi hayo umewezeshwa na kuwepo huduma za kifedha kupitia simu za mkononi ambazo zinatolewa na makampuni yanayotoa huduma za simu za mkononi nchini.

 

Makala hii imetayarishwa na Vodacom Foundation Tanzania

Tags: BoTM-PesaVodacom
Athanas Lupatu

Athanas Lupatu

Next Post
Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Ephraim Kwesigabo.

Mfumuko wa bei wapanda

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In