• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Tanzania Kuendelea kuimarisha biashara na Malawi

Patricia Richard by Patricia Richard
June 8, 2018
in BIASHARA
0
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla, kulia akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kongamano la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Malawi litakalofanyika Julai 26 na 27 jijini Mbeya, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) John Mnali.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla, kulia akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kongamano la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Malawi litakalofanyika Julai 26 na 27 jijini Mbeya, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) John Mnali.

Share on FacebookShare on Twitter

Na Fatma Salum-MAELEZO

Serikali ya Tanzania inaendelea na jitihada za kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na Serikali ya Malawi kupitia sekta ya biashara na uwekezaji ili wananchi waweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana katika nchi zote mbili.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, leo Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla alisema kuwa katika kuimarisha uhusiano huo, Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Malawi zimeandaa Kongamano la Biashara na Uwekezaji litakalofanyika Julai 26 na 27 mwaka huu Jijini Mbeya.

Makalla alieleza kuwa lengo la kongamano hilo ni kuwakutanisha wafanyabiashara na wawekezaji wan chi zote mbili ili kubaini fursa mbalimbali zitakazowezesha kuanzisha na kuendeleza miradi katika sekta za viwanda, usafirishaji, utalii, uvuvi, kilimo, madini, elimu, afya, benki, mawasiliano, Tehama na biashara kwa ujumla.

“Kongamano hili linatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki wapatao 500 ikijumuisha wafanyabiashara, wawekezaji, Taasisi za Umma na sekta binafsi kutoka Tanzania na Malawi,” alisema Makala.

ADVERTISEMENT

Sambamba na kongamano hilo, kutakuwepo mikutano ya wafanyabiashara (B2B), mikutano ya watendaji wa Serikali (G2G) na mikutano kati ya Serikali na wafanyabiashara (B2G) kutoka nchi zote mbili.

Makalla alisisitiza kuwa Mkoa wa Mbeya uko tayari kuchangamkia fursa za kibiashara na Malawi kwa sababu miundombinu ipo ya kutosha ikiwemo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe, meli mbili za kubeba mizigo ambazo zimeshaanza kufanya kazi na meli moja ya abiria ambayo itakamilika Julai mwaka huu.

Aidha, alibainisha kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa kuanza ujenzi wa kituo kimoja cha forodha (One Stop Boarder Post) katika mpaka wa Kasumulu na imetenga eneo la kujenga bandari kavu katika eneo la Inyala kwa lengo la kuwezesha upokeaji na uhifadhi wa bidhaa moja kwa moja kutoka bandari ya Dar es Salaam.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji (TIC), John Mnali alisisitiza kuwa kongamano hilo ni muhimu kwa wafanyabiashara wa kitanzania hivyo wajitokeze kushiriki ili waweze kuibua fusra mpya na kujitangaza kwa wenzao wa Malawi.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Godfrey Simbeye alitoa wito kwa wafanyabiashara wote hasa sekta binafsi kujitokeza kwa wingi kuangalia fursa zilizopo Malawi na kubadilishana uzoefu wa kibiashara.

Ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji (TIC), Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TanTrade) na Taasisi ya Biashara na Uwekezaji ya Malawi (MITC) wanaratibu kongamano hilo na mgeni rasmi atakuwa Makamu wa Rais wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan.

MWISHO.

Tags: biasharaMalawimbeyaMITCTICTPSFuwekezaji
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

TRA yadhamiria kupambana na biashara za magendo

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In