• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Monday, January 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Tengeneza fedha kupitia sekta ya ujenzi

Patricia Richard by Patricia Richard
August 31, 2018
in BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Ujenzi ni moja kati ya sekta kubwa nchini Tanzania. Sekta hii imeweza kuajiri watu wengi ambao wamekuwa wakiendesha maisha yao kupitia shughuli hiyo. Zipo shughuli nyingi zinazohitaji ujuzi wa darasani na taaluma ya kutosha ili kuziendesha, lakini ujenzi ni moja kati ya sekta ambayo imeweza kuajiri watu wengi walio wasomi na wasio wasomi. Kitu kikubwa ni kuhakikisha kazi yako inaonekana bora na ya kupendezesha, pia yenye kukubalika kwa maana ya kukidhi viwango.

Yawezekana una mtaji na haujui namna gani unaweza kuwekeza ili mtaji wako ukupatie faida zaidi. Leo tumekuletea fursa kumi za kibiashara zinazopatikana kupitia shughuli au huduma za ujenzi.

Ubunifu wa ramani (Uchoraji) na michoro ya majengo

Soma Pia  Ujenzi holela waweka watumishi matatani

Hzii ni moja kati ya fursa ambazo zimekuwa zikiwaingizia watu pesa nyingi sana. Kuna mtu anahitaji kujenga na anatamani kuwa na nyumba yenye ramani nzuri na muonekano tofauti na nyumba nyingine zinazomzunguka basi anahitaji hawa watu. Wachoraji ramani wameweza na na michoro wameweza kufanikisha ujenzi wa miradi mikubwa ikiwemo shule, vyuo, na ofisi mbalimbali za serikali zenye muonekano mzuri na wa tofauti kabisa.

Uuzaji wa vifaa

Shughuli ya ujenzi inahitaji vifaa vya kutosha hivyo kama unaona maeneo uliyopo yana shughuli nyingi zinazohusu ujenzi na una mtaji wa kutosha kuwekeza, ni muda wako kufanya hivyo,. Biashara hii inatajwa kuwaingizia faida kubwa wafanyabiashara.

Ufungaji wa vifaa vya usalama

ADVERTISEMENT

Biashara hii imekuwa ikikua kwa kasi kubwa hasa katika miji mikubwa kama vile Dar es salaam, Arusha, Mwanza, Tanga, Mbeya na Dodoma. Ufungaji huu unajumuisha, kamera za usalama, uzio wa umeme, uwekaji kengele n.k  Watu wengi baada ya kujenga wanapenda kujihakikishia usalama wa kutosha. Hivyo kamera nyingi zimekuwa zikifungwa kwa ajili ya kumwezesha mmiliki wa nyumba kujua usalama wa nyumbani kwake hata anapokuwa ametoka katika maeneo ya nyumba yake.

Soma Pia Ujenzi kuajiri 500 Dodoma

Upakaji rangi na mapambo

Watu wengi wanapenda nyumba zao zipendeze ziwe katika hali ya kuvutia. Rangi inachukua nafasi kubwa katika kupendezesha nyumba. Hii ni fursa ambayo ukiifanya kupitia hiyo utatengeneza pesa nyingi, kikubwa ni ufanisi na ubora katika nyumba taaluma hiyo. Ni jambo la kawaida kwa jirani kumuuliza mwenzake nani kapaka rangi nyumba yako, hivyo ni vema kufanya kazi kwa ubora wa hali ya juu, kwa sababu mteja mmoja anaweza kukuletea wateja kumi lakini pia anaweza kukupotezea wateja kumi. Vivyo hivyo katika upande wa upambaji, uwekaji wa taa nzuri, utengenezaji bustani ni kati ya fursa zinazowaingizia watu pesa.

Uuzaji na usambazaji wa chakula

Ujenzi ni kazi inayohitaji nguvu kubwa hivyo suala la chakula kwa wajenzi linapewa kipaumbele kikubwa. Zipo kampuni za ujenzi ambazo zimekuwa zikiingia mkataba na kampuni za usambazaji chakula ili kuwarahisishia wafanyakazi wao kupata chakula katika maeneo yao ya kazi. Fursa hii ni kubwa endapo utapika chakula kizuri na chenye kuzingatia mazingira ya usafi.

 

Tags: biasharaujasiriamaliujenzi
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Flyover yazalisha ajira 700

Discussion about this post

Habari Mpya

Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

January 30, 2023

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

January 30, 2023

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

by Pesatu Reporter
January 30, 2023
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amewasihi mashabiki wa Simba wamtie nguvu Mwekezaji Mohammed Dewji (Mo Dewji) kwa...

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

by Pesatu Reporter
January 30, 2023
0

Rais Samia amesema Serikali imetenga hadi eka 10 kwa kila kijana mwenye sifa za kufanya kilimo nchini Tanzania ili kuiwezesha...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In