• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, January 29, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Bila maji, uchumi wa viwanda ni ndoto

Patricia Richard by Patricia Richard
June 4, 2018
in MIUNDOMBINU
0
Share on FacebookShare on Twitter

Tanzania imeipokea kwa mikono miwili dhana ya kubadilisha nchi yetu kuwa ya uchumi wa viwanda. Mpaka hivi sasa kumekuwa na mabadiliko mbalimbali katika sekta ya viwanda ambayo serikali kwa kushirikiana na wadau wengine wamependekeza ili kukabiliana na changamoto mbalimbali za viwanda vya hapa nchini. Moja kati ya changamoto kubwa katika kuboresha viwanda hapa nchini ni upatikanaji wa maji. Ukweli ni kwamba viwanda haviwezi kusonga mbele bila uwepo wa maji ya uhakika. Sekta ya viwanda inategemea maji ili kufanikisha shughuli zake na kusaidia ukuaji wa uchumi. Hivyo basi ni muhimu kujiuliza, miundombinu ya maji iliyopo hivi sasa inaendana na kasi ya uboreshwaji wa viwanda?

Tayari serikali imeweka wazi kuwa imedhamiria kubadilisha uchumi na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda ifikapo mwaka 2025. Ni ukweli kuwa nchi haiwezi kuendelea bila sekta ya viwanda. Lakini tumejipangaje kuboresha viwanda vya hapa nchini? Wizara ya maji imejipangaje kuhakikisha kuwa maji sio tena changamoto kwa viwanda na hata matumizi ya kawaida ya nyumbani? Huwezi kufanya kazi vizuri kama unaumwa kutokana na kunywa maji yasiyo salama hivyo athari za maji huanza moja kwa moja kwa mwananchi wa kawaida mpaka kufikia ngazi za kimaendeleo kama viwanda.

ADVERTISEMENT

Ili kufanikisha lengo la kufikia uchumi wa kati mwaka 2025 suala la maji halipaswi kuachwa nyuma. Wadau wa masuala ya maji wanatakiwa kushirikishwa kikamilifu ili serikali ifikie azma hii ya uchumi wa viwanda. Viwanda haviwezi kuendelea kuzalisha bidhaa bila maji. Hivyo ili kukuza uchumi kwa kasi kwa kupitia sekta hii ni lazima kuwe na mpango madhubuti ili kukabiliana na changamoto za maji zilizopo.

Awali katika Bunge la Bajeti 2017/2018 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Gerson Lwenge alisema sekta ya maji hapa nchini inakumbwa na changamoto mbalimbali na mojawapo kati ya hizo ni kupungua kwa rasilimali hiyo kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira unaoendelea kote nchini. Mabadiliko ya tabianchi na matumizi mabaya ya maji pia ni changamoto kubwa katika sekta hii.

Hivyo basi ili kufikia lengo la uchumi wa viwanda, ni muhimu kwa serikali pamoja na watanzania kwa ujumla kusimamia rasilimali za maji na kuhakikisha kuwa hakuna uharibifu unaoendelea ili kusaidia rasilimali hizo ziendelee kuwepo. Kama ambavyo wadau wa maendeleo walivyopokea hili la viwanda basi wanatakiwa pia kuhakikisha kuwa miundombinu yote ya maji inatunzwa na kutumika inavyotakiwa kwani bila ya kuwa na matumizi sahihi ya maji na kutunza vyake, Tanzania ya viwanda itabaki kuwa ndoto tu.

 

Tags: maendeleomajimiundombinuRasilimaliuchumiviwanda
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Tume ya Madini yazinduliwa

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In