• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Tuesday, June 28, 2022
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Bidhaa bandia zinafikaje sokoni?

Patricia Richard by Patricia Richard
June 22, 2018
in BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Kumekuwa na ongezeko kubwa la bidhaa bandia hapa nchini, jambo ambalo limekuwa likiwapa wasiwasi wananchi. Mamlaka husika zimekuwa zikifanya kazi kubwa kudhibiti tatizo hili kwa kuwa na wakaguzi kote nchini ili kupambana na wanaofanya vitendo hivi lakini bado wanaonekana kuzidiwa nguvu kwani bado tumeendelea kushuhudia bidhaa hizi zikiteketezwa kila siku.

Lakini kama mamlaka zipo kuchunguza na kuangalia ubora wa bidhaa ni vipi bidhaa hizi zinaingia mitaani? Wahusika wanazidiwa nguvu? Hadi sasa kuna waliochukuliwa hatua za kisheria? Wananchi nao wanatoa mchango gani kutatua suala hili?

ADVERTISEMENT

Uwepo wa bidhaa hizi unahatarisha afya za wananchi ambao wengi wao wanashindwa kufahamu tofauti moja kwa moja, hali ambayo hupelekea mtu kununua bidhaa ambayo huenda ikasababisha matatizo ya kiafya. Mbali na hayo, uwepo na bidhaa bandia unasababisha hasara kwani mtu hutumia gharama kupata bidhaa fulani lakini baadae analazimika kuingia gharama nyingine tena ili kupata bidhaa hiyo hiyo yenye uhalali uliodhibitishwa.

Swali linakuja, baada ya mamlaka kukamata watu hawa wanaojihusisha na usambazaji wa bidhaa bandia, nini kinafuata? Hatua gani zinachukuliwa? Wanaadhibiwa kwa mujibu wa sheria? Mamlaka hizi zinachukua hatua gani kuhakikisha kuwa tatizo hili linapata suluhisho la kudumu? Wananchi wanaelimishwa vya kutosha kuhusu bidhaa bandia?

Uingizwaji wa bidhaa bandia unapaswa kudhibitiwa na kupewa kipaumbele zaidi. Ulinzi uimarishwe katika bandari, mipaka na viwanja vyote vya ndege. Hatua kali zaidi za kisheria zichukuliwe kwa wafanyabiashara pamoja na wote ambao kwa namna moja au nyingine wanachangia katika mtandao huo. Vilevile, TFDA pamoja na TBS wanapaswa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ambazo unaweza kugundua bidhaa isiyo halali kabla ya kuinunua na kutumia. Vianzishwe vituo ambavyo vitakuwa vinapokea malalamiko au taarifa kutoka kwa wananchi ili kuzuia athari zaidi zinazotokana na matumizi ya bidhaa hizi.

Wataalamu wanatakiwa kuhakikisha wanafanya ukaguzi mara kwa mara ili uwezekano wa wafanyabiashara kuweka sokoni bidhaa zisizofaa uwe mdogo. Washtukize zoezi hili mara kwa mara. Kufanya hivi kutapunguza tatizo hili na kuwaepusha wananchi na usumbufu wa aina yoyote kwa kiasi kikubwa. Tanzania bila bidhaa banda inawezekana. Wananchi wazidi kushirikiana na mamlaka husika ili kuhakikisha kuwa tatizo hili linapatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Tags: TBSTFDAwafanyabiashara
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Kilimo cha alizeti kisiachwe nyuma

Discussion about this post

Habari Mpya

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

June 28, 2022

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

June 28, 2022

Mapendekezo bima ya afya kwa wote

June 28, 2022

Turkish Airlines yarejesha safari zake KIA

June 28, 2022
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla akizungumza katika warsha ya viongozi wa Serikali wa mkoa na Bank ya NMB.

Benki ya NMB yapongezwa

June 28, 2022

Rais Samia azindua taasisi Zanzibar

June 28, 2022

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Kilimo biashara, sekta yenye fursa za uwekezaji

by Jensen Kato
June 28, 2022
0

Kilimo biashara kinaendelea kukua barani Afrika na muda umefika kwa watu hususani vijana kuchagamkia fursa mbalimbali zinazotokana na kilimo. Watu...

Miamala ya simu yaongeza Pato la Taifa

by Pesatu Reporter
June 28, 2022
0

Miamala ya fedha kwa njia ya simu imechangia kuongezeka kwa pato la Taifa kutoka asilimia 40 mwaka 2013 hadi kufikia...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2022 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In