• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Monday, January 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Kilimo cha alizeti kisiachwe nyuma

Patricia Richard by Patricia Richard
June 22, 2018
in KILIMO
0
Share on FacebookShare on Twitter

Kumekuwa na jitihada zinazoendelea kujaribu kukinusuru kilimo kwa kusambaza mbegu bora. Juhudi hizi hasa zimeelekezwa kwenye mazao ya chakula Kama vile mahindi, viazi na mtama. Baadhi ya kampuni zinasambaza mbegu na kuwasimamia wakulima wa mazao yanayotengeneza bidhaa zao mfano bia. Mashirika ya kimataifa nayo yanatoa msukumo wake kuhakikisha Afrika inakuwa na mchango unaostahili katika kujitosheleza kwa chakula.

Juhudi hizo pia zipo kwenye kilimo na usindikaji au ukamuaji wa alizeti nchini. Kwa upande mmoja, jitihada hizi zimekusudia kuvilinda viwanda vya kukamua na kusafisha mafuta ya alizeti visizidiwe nguvu na kumezwa kabisa na vile vya kusafisha na kusindika mafuta ghafi ya mawese ambayo uagizaji wake kutoka nje umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka.

Uagizaji huu umekuwa ukihatarisha uhai na ustawi wa alizeti pamoja na kilimo cha michikichi nchini. Hata hivyo, jitihada za maboresho hayo kwa kiasi kikubwa yametokana na msukumo na ushawishi wa wafadhili kuliko jitihada zetu wenyewe.

Hili linasababisha mipango mingi kutokuwa endelevu mara tu wafadhili wanapojitoa au misaada ya kufadhili mradi kukoma. Mifano ipo mingi nchini. Kwa kipindi kirefu, kilimo cha alizeti na mbegu nyingine za mafuta ya kula kimegubikwa na maneno yenye nadharia zaidi kuliko sayansi, bila ya mipango thabiti yenye tija na utekelezaji.

Mipango mingi imekosa ufuatiliaji wa karibu na kwa kiasi kikubwa, utekelezaji wake katika maeneo kadhaa ulibakia kwenye karatasi kutokana na changamoto mbalimbali kwa kukosa mifumo shirikishi kukiendeleza kilimo cha alizeti nchini.

Pamoja na umuhimu wake kiuchumi na kibiashara, zao la alizeti kwa kipindi kirefu limekuwa likipuuzwa na kuchukuliwa kama moja ya mazao ya kukumbukwa wakati wa njaa au shida.

Umuhimu wa kibiashara umeelekezwa kwenye mazao yaliyozoeleka mfano pamba, tumbaku, chai, korosho, karafuu, mkonge, pareto na kahawa. Alizeti imeshaulika kiasi cha kutopangiwa mikakati na malengo ya kuliendeleza. Kilimo cha alizeti kwa kiasi kikubwa kinaendeshwa na wakulima wadogo, kimekuwa kikifanywa kwa kubahatisha kutokana na sababu mbalimbali hivyo kuwa na mavuno hafifu na kiwango kidogo cha mafuta katika mbegu zake.

ADVERTISEMENT

Wakati kwingineko duniani kukiwa na jitihada za makusudi za kuboresha na kuongeza uzalishaji wa alizeti na ukamuaji wa mafuta bora zaidi ambayo ni salama kwa kwa matumizi ya binadamu (kama mafuta ya kupikia), jitihada kama hizo zinakosekana nchini kwa kipindi kirefu sasa.

Hivi karibuni wamejitokeza wafadhili ambao wamejipanga kuwajengea uwezo wakulima kuweka msisitizo kwenye kilimo hiki hivyo kuanza kutoa mwelekeo wa kuliendeleza zao hili katika kipindi cha miaka 20 ijayo.

Lakini mchango huo wa wafadhili bila ya jitihada za makusudi za Serikali na taasisi zake kusimamia utafiti wa mbegu bora, upatikanaji wa mbegu hizo kwa bei nafuu au kwa mikopo yenye ruzuku na udhibiti wa wanunuzi wakati wa mavuno ya mbegu hizo kabla ya usindikaji hautakuwa na maana yoyote.

Ipo haja kwa wadau kuunga mkono jitihada hizi kwa kurahisisha upatikanaji wa mashine za teknolojia ya kisasa katika kukamua mafuta na kuyasafisha ambazo itakuwa nafuu zaidi zikipata msamaha wa kodi na upatikanaji wa vifungashio vyenye ubora wa kimataifa.

Mamlaka husika zinatakiwa kuongeza umakini na uwajibikaji kama ile ya Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) au Shirika la Viwango nchini (TBS) kudhibiti uchakachuaji wa mafuta kwa kufuatilia kwa karibu uwezekano wa kuchanganywa na mawese kwa lengo la kutengeneza faida kubwa kwa njia za mkato.

Umakini unahitajika pia katika kudhibiti uwiano wenye tija baina ya uagizaji na uingizaji wa mafuta ghafi ya mawese kutoka nje na kiwango cha uzalishaji wa mafuta ya alizeti nchini kwa kudhibiti kiasi cha alizeti ghafi zinazouzwa nje ya nchi.

Serikali inapaswa kujenga mazingira rafiki kwa wakulima na wadau wengine wa kilimo cha alizeti na wasindikaji wake kwa kuondoa tozo, ushuru na kodi ambazo ni kikwazo kwa sekta hiyo kuongeza ushindani wake katika soko la kimataifa. Vilevile idhibiti mianya ya rushwa katika uingizaji wa mafuta ya mawese na kuhakikisha sehemu kubwa ya yanayoingia inatumika kwa ajili ya kutengenezea bidhaa zitakazouzwa nje na kidogo kinachobaki kitumike kusafisha mafuta ya kupikia nchini kwa kuwa na vifungashio maalum.

 

Tags: AlizetikilimomafutaTBSTFDA
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Umri usiwe kikwazo cha maendeleo

Discussion about this post

Habari Mpya

Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

January 30, 2023

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

January 30, 2023

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Mohammed Dewji (Mo Dewji). Picha|Mtandao

Watieni nguvu wawekezaji: Makalla

by Pesatu Reporter
January 30, 2023
0

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Amos Makalla amewasihi mashabiki wa Simba wamtie nguvu Mwekezaji Mohammed Dewji (Mo Dewji) kwa...

Vijana Tanzania kupatiwa eka 10 kulima

by Pesatu Reporter
January 30, 2023
0

Rais Samia amesema Serikali imetenga hadi eka 10 kwa kila kijana mwenye sifa za kufanya kilimo nchini Tanzania ili kuiwezesha...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In