• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, September 24, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Kilimo cha alizeti kisiachwe nyuma

Patricia Richard by Patricia Richard
June 22, 2018
in KILIMO
0
Share on FacebookShare on Twitter

Kumekuwa na jitihada zinazoendelea kujaribu kukinusuru kilimo kwa kusambaza mbegu bora. Juhudi hizi hasa zimeelekezwa kwenye mazao ya chakula Kama vile mahindi, viazi na mtama. Baadhi ya kampuni zinasambaza mbegu na kuwasimamia wakulima wa mazao yanayotengeneza bidhaa zao mfano bia. Mashirika ya kimataifa nayo yanatoa msukumo wake kuhakikisha Afrika inakuwa na mchango unaostahili katika kujitosheleza kwa chakula.

Juhudi hizo pia zipo kwenye kilimo na usindikaji au ukamuaji wa alizeti nchini. Kwa upande mmoja, jitihada hizi zimekusudia kuvilinda viwanda vya kukamua na kusafisha mafuta ya alizeti visizidiwe nguvu na kumezwa kabisa na vile vya kusafisha na kusindika mafuta ghafi ya mawese ambayo uagizaji wake kutoka nje umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka.

Uagizaji huu umekuwa ukihatarisha uhai na ustawi wa alizeti pamoja na kilimo cha michikichi nchini. Hata hivyo, jitihada za maboresho hayo kwa kiasi kikubwa yametokana na msukumo na ushawishi wa wafadhili kuliko jitihada zetu wenyewe.

Hili linasababisha mipango mingi kutokuwa endelevu mara tu wafadhili wanapojitoa au misaada ya kufadhili mradi kukoma. Mifano ipo mingi nchini. Kwa kipindi kirefu, kilimo cha alizeti na mbegu nyingine za mafuta ya kula kimegubikwa na maneno yenye nadharia zaidi kuliko sayansi, bila ya mipango thabiti yenye tija na utekelezaji.

Mipango mingi imekosa ufuatiliaji wa karibu na kwa kiasi kikubwa, utekelezaji wake katika maeneo kadhaa ulibakia kwenye karatasi kutokana na changamoto mbalimbali kwa kukosa mifumo shirikishi kukiendeleza kilimo cha alizeti nchini.

Pamoja na umuhimu wake kiuchumi na kibiashara, zao la alizeti kwa kipindi kirefu limekuwa likipuuzwa na kuchukuliwa kama moja ya mazao ya kukumbukwa wakati wa njaa au shida.

Umuhimu wa kibiashara umeelekezwa kwenye mazao yaliyozoeleka mfano pamba, tumbaku, chai, korosho, karafuu, mkonge, pareto na kahawa. Alizeti imeshaulika kiasi cha kutopangiwa mikakati na malengo ya kuliendeleza. Kilimo cha alizeti kwa kiasi kikubwa kinaendeshwa na wakulima wadogo, kimekuwa kikifanywa kwa kubahatisha kutokana na sababu mbalimbali hivyo kuwa na mavuno hafifu na kiwango kidogo cha mafuta katika mbegu zake.

Wakati kwingineko duniani kukiwa na jitihada za makusudi za kuboresha na kuongeza uzalishaji wa alizeti na ukamuaji wa mafuta bora zaidi ambayo ni salama kwa kwa matumizi ya binadamu (kama mafuta ya kupikia), jitihada kama hizo zinakosekana nchini kwa kipindi kirefu sasa.

Hivi karibuni wamejitokeza wafadhili ambao wamejipanga kuwajengea uwezo wakulima kuweka msisitizo kwenye kilimo hiki hivyo kuanza kutoa mwelekeo wa kuliendeleza zao hili katika kipindi cha miaka 20 ijayo.

Lakini mchango huo wa wafadhili bila ya jitihada za makusudi za Serikali na taasisi zake kusimamia utafiti wa mbegu bora, upatikanaji wa mbegu hizo kwa bei nafuu au kwa mikopo yenye ruzuku na udhibiti wa wanunuzi wakati wa mavuno ya mbegu hizo kabla ya usindikaji hautakuwa na maana yoyote.

Ipo haja kwa wadau kuunga mkono jitihada hizi kwa kurahisisha upatikanaji wa mashine za teknolojia ya kisasa katika kukamua mafuta na kuyasafisha ambazo itakuwa nafuu zaidi zikipata msamaha wa kodi na upatikanaji wa vifungashio vyenye ubora wa kimataifa.

ADVERTISEMENT

Mamlaka husika zinatakiwa kuongeza umakini na uwajibikaji kama ile ya Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) au Shirika la Viwango nchini (TBS) kudhibiti uchakachuaji wa mafuta kwa kufuatilia kwa karibu uwezekano wa kuchanganywa na mawese kwa lengo la kutengeneza faida kubwa kwa njia za mkato.

Umakini unahitajika pia katika kudhibiti uwiano wenye tija baina ya uagizaji na uingizaji wa mafuta ghafi ya mawese kutoka nje na kiwango cha uzalishaji wa mafuta ya alizeti nchini kwa kudhibiti kiasi cha alizeti ghafi zinazouzwa nje ya nchi.

Serikali inapaswa kujenga mazingira rafiki kwa wakulima na wadau wengine wa kilimo cha alizeti na wasindikaji wake kwa kuondoa tozo, ushuru na kodi ambazo ni kikwazo kwa sekta hiyo kuongeza ushindani wake katika soko la kimataifa. Vilevile idhibiti mianya ya rushwa katika uingizaji wa mafuta ya mawese na kuhakikisha sehemu kubwa ya yanayoingia inatumika kwa ajili ya kutengenezea bidhaa zitakazouzwa nje na kidogo kinachobaki kitumike kusafisha mafuta ya kupikia nchini kwa kuwa na vifungashio maalum.

 

Tags: AlizetikilimomafutaTBSTFDA
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Umri usiwe kikwazo cha maendeleo

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

September 14, 2023

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

September 14, 2023
Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande.

Tanzania yapiga hatua utakatishaji fedha

September 12, 2023
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Picha| Ikulu

Tutawaunganisha wakulima na soko: Rais Samia

September 11, 2023

Mbaazi yaleta neema kwa wakulima 2023

September 7, 2023

Bei za mafuta zapanda tena Tz

September 6, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Tanzania ni nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali barani Afrika na inashika nafasi ya 14 dunia. Ethiopia, ndio nchi...

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Benki ya Exim imezindua ushirikiano wa kimkakati na Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na kufanya mafunzo ya...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In