• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Umuhimu wa Logo katika biashara

Patricia Richard by Patricia Richard
July 12, 2018
in BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Katika biashara, kuna vitu muhimu ambavyo mjasirimali/mfanyabiashara lazima avizingatie kabla hajaanzisha biashara yake mbali na kuwa na mtaji, vitendea kazi eneo la biashara, soko n.k. Kwa jamii nyingi za Afrika Mashariki, walio wengi wamekuwa wakifanya biashara na biashara zao kufanikiwa kwa kiasi kikubwa tu lakini bado wamekosa kitu kimoja cha muhimu sana.

Wajasiriamali wadogo wadogo na baadhi ya wafanyabiashara hawana nembo zao za biashara maarufu kama Logo.

Nembo ya Biashara (Logo) ni nini na inamsaidia vipi mfanyabiashara/mjasiriamali?

Kwa tafsiri rahisi, nembo ni alama zinazoundwa na maandishi na picha ambazo zinatusaidia kutambua bidhaa au huduma tunayopenda kwa kuwasaidia wateja kuelewa nini unachofanya, wewe ni nani na unaamini nini na matarajio yako ni yapi.

Kuna umuhimu mkubwa wa mfanyabiashara au mjasiriamali kumiliki au kuwa na nembo ya biashara.

Unaweza kuwa na biashara nzuri tu ya utoaji huduma au bidhaa lakini watu wasivutike na biashara yako wakaenda sehemu nyingine kununua kwa sababu tu wamependezwa na nembo ya mfanyabiashara mwenzako kutokana na dhima au ujumbe uliopo.

Kwanini unashauriwa kumiliki au kuwa na nembo ya biashara?

Nembo ya biashara ni utambulisho wako. Kitu kitakachoitambulisha biashara yako au huduma yako bila kujali kama ni bidhaa iko katika uzito au ujazo gani na kama ni huduma haitajalisha inatolewa sehemu gani ni nembo. Nembo inatengeneza hisia, fikra, mwamko na hamasa ya kununua huduma au bidhaa kwa mteja. Kwa mfano ni kawaida kusikia mtu akisema nimeona matangazo ya kampuni fulani kwani imefika hadi huku? Mara nyingi kitu cha kwanza kujiuliza itakuwa ni nembo ya kampuni au biashara.

Nembo inasaidia kuonyesha umaridadi na ufanisi wa kampuni. Kampuni yoyote yenye kuhitaji kufanya kazi kwa ufanisi lazima iwe na logo (nembo). Nembo inasaidia kuonyesha uthubutu na umakini wa kampuni au biashara ambayo yaweza kuwa ni ya utoaji huduma au uzalishaji wa bidhaa.

Nembo inabeba ujumbe wa biashara yako. Ujumbe ni muhimu katika nembo yako kwa sababu inabeba kile ambacho kampuni yako inafanya. Ujumbe mara nyingi huwa ni wenye mvuto na utakaowafanya wateja wako kuvutika na kuja kuhudumiwa au kununua bidhaa zako- Mathalani unamiliki duka la mapambo linaitwa “Mwanamapambo” Kisha ukaweka ujumbe huu “ Unajenga tunakusaidia kupamba” Ujumbe tu umeshabeba kile unachokifanya ambacho ni uuzaji wa mapambo mtu hatokuwa na haja ya kuja kuuliza duka lako linahusiana na mapambo ya aina gani.

Nembo inasaidia kuonyesha umiliki. Nembo ni moja kati ya alama zinazoonyesha umiliki wa biashara kwa sababu nembo hubeba jina la kampuni au mmiliki wa kampuni. Mfano Azam, Kiluswa Company Limited, Kafulusu Enterprises na mengineyo. Majina hayo yanaonyesha mmiliki wa kampuni ni nani.

ADVERTISEMENT

Nembo inasaidia kuonyesha matarajio ya biashara. Nembo inasaidia kubeba maono na muelekeo wa biashara yako na hasa kwa kuwaonyesha wateja watarajie nini huko mbele kutokana na huduma au bidhaa unazotoa. Hii inasaidia biashara yako kuwa na ushindani dhidi ya kampuni nyingine zinazotoa huduma kama yako. Mfano kampuni za mawasiliano. Maneno kama “Yajayo yanafurahisha! Uko tayari” yanasaidia kuwafanya wateja wa kampuni kuendelea kusubiria mambo mazuri ambayo kampuni yao imewaahidi.

Nembo ya biashara (logo) ina umuhimu mkubwa katika kutambulisha biashara sokoni hivyo ni vema mfanyabiashara au mjasiriamali kuwa na logo kwa sababu itakusaidia kujitofautisha na wafanyabiashara wengine wanaofanya biashara kama yako. Nembo inasaidi sana kuonyesha uthamani wa biashara unayoifanya.

 

Tags: biasharaMjasiriamaliNembosoko
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Wanawake Monduli wazindua kiwanda cha ngozi

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In