• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, September 24, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

WAFANYABIASHARA DAR ES SALAAM WAELIMISHWA KUHUSU KODI YA ZUIO

kodi hiyo ambayo ni asilimia 10 ya kiasi cha malipo walichokubaliana katika mkataba wa upangishaji ili waiwasilishe TRA.

Jensen Kato by Jensen Kato
June 12, 2020
in BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter
ADVERTISEMENT
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewaelimisha wafanyabiashara wa maeneo ya Tabata jijini Dar es Salaam kuhusu Kodi ya Zuio na kutoa wito kwa wamiliki wa majengo, fremu na ardhi kuwaruhusu wapangaji wao kuzuia kodi hiyo ambayo ni asilimia 10 ya kiasi cha malipo walichokubaliana katika mkataba wa upangishaji ili waiwasilishe TRA.

Akizungumza wakati wa kampeni endelevu ya elimu kwa mlipakodi ambayo kwa awamu hii itamalizika kesho jijini hapa, Afisa Msimamizi Mkuu wa Kodi kutoka Mamlaka hiyo Bw. Stephen Kauzeni alisema kuwa, kodi ya zuio inatozwa kwa mujibu wa Sheria ya Kodi ya Mapato na inasimamiwa na TRA hivyo amewataka wapangishaji kuwaruhusu wapangaji wao kuzuia kodi hiyo wakati wanapolipwa kodi ya pango.

“Tangu tumeanza zoezi hili la elimu kwa mlipakodi tumefanikiwa kupita karibu maeneo yote ya Tabata ikiwa ni pamoja na Relini, Bima, Barakuda, Kimanga, Kisukulu na Kinyerezi. Katika maeneo yote haya tumegundua kwamba, baadhi ya wamiliki wa nyumba za biashara hawaruhusu wapangaji wao kukata kodi ya zuio ambayo inapaswa kuwasilishwa TRA kwa mujibu wa sheria.

“Tulichokifanya ni kuwaelimisha wafanyabiashara kuhusu umuhimu wa kodi hiyo na napenda kuchukua fursa hii kutoa wito kwa wenye nyumba na fremu mbalimbali kuwaruhusu wapangaji wao kuzuia asilimia 10 ya kiasi cha malipo walichokubaliana kwenye mkataba wa upangishaji ili wapangaji hao wakiwasilishe Mamlaka ya Mapato Tanzania,” alisema Bw. Kauzeni.

Bw. Rashid Omary ni mmiliki wa fremu za biashara wa Tabata Kimanga jijini hapa ambaye amesema kuwa, amefurahishwa na elimu ya kodi ya zuio aliyoipata kutoka kwa maafisa wa TRA na amewaomba wamiliki wenzake kuhakikisha wanawaruhusu wapangaji wao kuzuia asilimia 10 ya kodi ya pango ili fedha hizo ziwasilishwe TRA kama sheria inavyoelekeza.

“Kama mimi ni mmiliki lakini nilikuwa sielewi kama wapangaji wangu wanatakiwa kunikata asilimia 10 ya kodi ya pango tuliyokubaliana kwenye mkataba ili waipeleke TRA. Hivyo elimu hii imenifungua sana na hivyo napenda kuwashauri wamiliki wenzangu wawaruhusu wapangaji wao kukata hiyo asilimia 10 kwa sababu kodi hii itarudi kwetu kupitia maendeleo yanayoletwa na Serikali katika maeneo yetu tunayoishi, alisema Bw. Omary.

Naye, mmiliki wa maduka ya Ikupa Market Bi. Hortensia Kimaro ameiomba Mamlaka ya Mapato Tanzania iwasajili wenye majengo ya biashara ili walipe kodi ya zuio wao wenyewe kwa sababu baadhi yao ni wagumu kuwaruhusu wapangaji wao kuzuia kodi hiyo.

Kodi ya zuio hutozwa katika maeneo tofauti ikiwa ni pamoja na malipo ya mishahara, mirabaha, hisa, upangishaji na gawio mbalimbali ambapo kila eneo limepangiwa kiwango cha asilimia kinachotakiwa kulipwa.

Jensen Kato

Jensen Kato

Next Post
International Monetary Fund logo is seen outside the headquarters building during the IMF/World Bank spring meeting in Washington, U.S., April 20, 2018. REUTERS/Yuri Gripas

IMF YATOA DOLA MILIONI 14.3 KWA TANZANIA

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

September 14, 2023

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

September 14, 2023
Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande.

Tanzania yapiga hatua utakatishaji fedha

September 12, 2023
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Picha| Ikulu

Tutawaunganisha wakulima na soko: Rais Samia

September 11, 2023

Mbaazi yaleta neema kwa wakulima 2023

September 7, 2023

Bei za mafuta zapanda tena Tz

September 6, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Tanzania ni nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali barani Afrika na inashika nafasi ya 14 dunia. Ethiopia, ndio nchi...

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Benki ya Exim imezindua ushirikiano wa kimkakati na Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na kufanya mafunzo ya...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In