• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, January 29, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Jinsi pombe inavyochochea umaskini

Patricia Richard by Patricia Richard
July 19, 2018
in FEDHA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Pombe imekuwa changamoto katika kufikia malengo sio tu hapa nchini bali duniani kote kwa ujumla. Vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa wameathirika na matumizi ya pombe kupita kiasi. Unywaji wa pombe uliokithiri umekuwa chanzo cha watu wengi sio tu vijana kuendelea kuwepo katika dimbwi la umaskini kwa sababu wamekuwa watumwa wa ulevi na wanaona maisha yao hayawezi kusonga bila pombe. Inapaswa kujiuliza, tutaweza kufikia nchi yenye uchumi wa kati kama tutaendelea kushuhudia pombe ikiteketeza nguvu kazi ya taifa bila kuchukua hatua yoyote?

Kundi kubwa la vijana huanza kujihusisha na ulevi wakiwa wadogo hivyo wanapata wakati mgumu kuacha mazoea haya kadri miaka inavyosonga. Tabia hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na watoto kukosa malezi mazuri kutoka kwa wazazi na familia na vile vile ushawishi kutoka kwa marafiki zao wa karibu. Ni kweli kuwa huwezi kuingilia maamuzi binafsi ya mtu na kumpiga marufuku kutumia kilevi endapo anatumia gharama zake mwenyewe. Lakini unywaji wa pombe uliokithiri haumuumizi mtu mmoja tu bali hata wale wa karibu yake na jamii kwa ujumla.

Kwa haraka tu tujiulize, mlevi ni mtu wa kuweka akiba? Ni mtu mwenye kutumia fedha zake kistaarabu? Ni mtunzaji wa familia? Hapana. Watu hawa hutafuta fedha na kuzimaliza zote sehemu za starehe. Hivyo maamuzi yao hayawaathiri wao tu bali hata wale ambao wanawategemea. Kama watoto watashindwa kupelekwa shuleni watakuwa na maisha gani kesho? Kama kila shilingi inayoingizwa inatumika kugharamia pombe, watoto hawa wataishi vipi kama hawajawekewa misingi imara na wale wanaowategemea?

ADVERTISEMENT

Unywaji pombe umekuwa sababu mojawapo ya watu wa hali ya chini kuendelea kuwa chini kutokana na kwamba, wanashindwa kutimiza mahitaji mengine muhimu au hata kuwekeza katika biashara sababu wanakosa muongozo wa namna na kutumia kile wanachopata. Matokeo yake, watu hawa wanashindwa kupambana na umaskini na hivyo wanabakia katika hali hiyo

Ulevi pia umekuwa chanzo cha migogoro katika familia na jamii kwa ujumla. Tumeshuhudia familia zikiiingia katika migogoro kutokana na hili. Mbali na kwamba migogoro hii mara nyingi huishia kuwaumiza zaidi watoto, familia kusambaratika na kukosa msaada waliokuwa wanaupata mwanzo kunaweza kuwaweka katika nafasi mbaya kiuchumi. Hivyo jambo hili sio la kufumbiwa macho. Ni lazima watu wenye matatizo ya kunywa kupita kiasi wasaidiwe. Starehe hii ikipitiliza, inawaumiza wengine.

Tags: akibafedhaPombeuchumiUmaskini
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
Stanbic Bank

Benki ya Stanbic yazindua kampeni ya ‘Zaidi ya Benki’

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In