• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Ubunifu wa Furniture ni fursa tosha

Patricia Richard by Patricia Richard
June 8, 2018
in UJASIRIAMALI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Kutokana na changamoto ya ajira nchini, vijana wengi wameamua kujiongeza na kuwa wabunifu. Ubunifu huu si tu kwa wasomi pekee, bali hata walioishia darasa la saba wamekua wakiufanya au kuiga wakiendeleza pale walipoishia wengine.

Moja ya faida ya kukosekana kwa ajira ni kukua kwa ubunifu hasa wa kibiashara na hivyo kupelekea kukua kwa biashara ya furniture za majumbani na hata maofisini. Biashara hii ilikua ikifanywa kwa uchache na mafundi seremala ambao walijikita zaidi katika kutengeneza vitu kama madirisha na milango huku furniture za ndani hasa sebuleni wakizipa umuhimu kiduchu.

Ushindani ni kitu kizuri na kinalipa, baada ya kuwapo kwa wimbi kubwa la vijana waliokimbilia ufundi stadi hasa useremala na hivyo kuongeza idadi ya mafundi mtaani na ushindani kukua, hali ambayo kwa kiasi kikubwa imepelekea ubunifu kuongezeka na jamii kuanza kupata matokeo chanya.

ADVERTISEMENT

Kupendeza kwa mandhari ya sebule na varanda za nyumba mbalimbali nchini ni matokeo ya ubunifu huu wa mafundi seremala. Vijana wengi wamejikita katika kutengeneza meza za kuwekea televisheni na maua, meza zakahawa (coffee table), meza za chakula (dining table), seti za masofa,vitanda vya wakubwa na watoto, makabati ya nguo na vyombo n k.

Biashara hii licha ya kutatua changamoto ya ajira, pia imeongeza kipato cha mtu na mtu, familia na taifa kwa ujumla.Ubunifu katika furniture umepelekea kuongezeka kwa soko la wanaozitumia hivyo baadhi ya vijana wameamua kuanzisha viwanda vidogo ambavyo vinaliingizia taifa kodi ya mapato.

Licha ya kukua na kupendwa kwa furniture hizi za mitaani, baadhi ya mafundi wamekuwa sio waaminifu kwa kuchukua pesa za wateja na kutokomea kusikojulikana ama kutokabidhi kazi kwa wakati kama inavyopaswa. Vijana wanatakiwa kuwa waaminifu kwa wateja, pia warasimishe biashara zao kwa kujenga jina na kuwa na eneo maalumu la kufanyia kazi(work shop) ili kuongeza uaminifu na ufanisi.

Tags: biasharaFurnituremapatoubunifuUfundi Stadi
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post

Uchafu wa mazingira waponza wamiliki wa viwanda Mikocheni

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In