• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, January 29, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

TIC yasema kukamilika kwa uwanja wa ndege jengo la tatu kutavutia wawekezaji wengi zaidi

Patricia Richard by Patricia Richard
October 5, 2018
in MIUNDOMBINU
0
Jengo jipya la tatu la Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere linavyoonekana kwa mbele likiwa limekamilika kwa asilimia 82 ya ujenzi wake, jengo hilo linagharimu zaidi ya shilingi bilioni 56 za kitanzania na linatarajia kukamilika ujenzi wake Mei 31 mwaka 2019.

Jengo jipya la tatu la Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere linavyoonekana kwa mbele likiwa limekamilika kwa asilimia 82 ya ujenzi wake, jengo hilo linagharimu zaidi ya shilingi bilioni 56 za kitanzania na linatarajia kukamilika ujenzi wake Mei 31 mwaka 2019.

Share on FacebookShare on Twitter

Na Grace Semfuko-MAELEZO.

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), kinatambua kuwa miezi michache ijayo serikali kwa kukamilisha ujenzi wa majengo na ufungaji wa mitambo ya kisasa kukidhi mahitaji ya teknolojia ya kimataifa, jengo la tatu (Terminal 3)  Uwanja wa Kimataifa Julius Nyerere( JNIA) ni ukurasa mpya wa fursa za kuongeza kasi ya  uwekezaji hapa nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa TIC, Geoffrey Mwambe alitembelea eneo la ujenzi na kupokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Anga Tanzania ( TAA), Richard Mayongela kwa ziara ya kutambua zaidi mapya ya jengo la tatu ili kumpa nafasi ya kujenga vishawishi kwa wawekezaji kuhusu manufaa ya chombo hicho kinachokamilika wakati tayari tatizo la foleni ya magari toka uwanjani huo kuingia jijini umeisha  baada ya barabara la juu kukamilika katika maungo ya barabara za Mandela toka bandarini na Nyerere itokayo JNIA.

TIC ni taasisi ya serikali, imekuwa ikifanya juhudi za kufafanua kwa wawekezaji fursa zilizopo Tanzania kwa lengo la kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje  nchi , na hivyo kukamilika kwa ujenzi wa uwanja huo na kuwa chombo chenye kila hitaji la abiria wa anga katika dunia ya sasa, utaongeza idadi ya wawekezaji  kwa sababu ya huduma mpya hizo. “Huduma yetu usafiri wa anga inabadilika kabisa” amesema Mkurugenzi Mkuu TAA, Mayongela.

Mayongela amesema kukamilika kwa uwanja huo mpya jengo la tatu kutaondoa kabisa msongamano wa abiria uliopo uwanja wa pili (Terminal 2) uliojengwa miaka 34 iliyopita, ambao kwa wakati huo ulilenga kuhudumia abiria Milioni 1.5 na sasa umezidiwa kwa kuhudumia abiria hadi milioni   2.5 kwa mwaka,  kutokana na ongezeko la abiria nahatimaye kusababisha kuzidiwa kwa uwanja huo.

ADVERTISEMENT

Uamuzi wa kujenga kituo cha pili (Terminal 2) ulioazimiwa na serikali mwaka 1984 ulitokana na kuwepo kwa ongezeko la abiria kituo la kwanza (Terminal 1) kilichojengwa mwaka 1956, ambapo kituo kilikuwa na uwezo wa kuhudumia abiria laki tano tu, hatua iliyosababisha Serikali kujenga uwanja huo wa pili ambao nao kwa sasa umelemewa na abiria wengi.

“Ujenzi wa uwanja huu ni mkombozi mkubwa kwetu watanzania katika kuboresha sekta ya anga,uwanja wa ndege tunaoutumia sasa ulijengwa mwaka 1984 ,ni miaka 34 mpaka sasa kwa hiyo utaona ni jinsi gani tulivyo bize kuhudumia abiria kwa idadi iliyolengwa mwaka huo kwa sasa watu tumeongezeka na hivyo serikali imefanya jambo la msingi sana kujenga uwanja huu” Alisema Mkurugenzi Mkuu TAA.

Hata hivyo, vituo viwili vilivyopo, uwanja huo JNIA bado vilikuwa na mapungufu ya mahitaji ya kisasa kwa dunia inayobadilika kila siku kiteknolojia, na Mkurugenzi Mkuu wa TIC ameelezwa huduma sasa zitakuwa na viwango vya kuhudumia kila aina ya makundi ya watu maarufu na kituo sasa kitaweza kupokea aina yoyote ya ndege pasipo kuhofia ubora ama ukubwa wake.

Kadhalika,  naye Bw. Mwambe amekiri na kufurahishwa na hatua za uboreshaji wa usafiri wa anga uliofikiwa na taifa na kuongeza kuwa kukamilika kwa uwanja huo kutasaidia kuongezeka kwa tija kwenye uwekezaji, kwani abiria na mizigo ya wawekezaji itahudumiwa kwa usafiri wa anga.

“Usafiri wa anga una uhusiano mkubwa na kuimarisha uwekezaji nchini,wawekezaji wengi wanaingia nchini kupitia usafiri wa anga,wanakuja na kuleta vifaa vya uwekezaji kwa kutumia usafiri wa aina mbalimbali ukiwepo usafiri huu wa anga,kwa hiyo kukamilika kwa uwanja huu kutatusaidia sisi kuimarisha sekta ya uwekezaji Nchini na ndio maana nimekuja kuangalia maendeleo yake” Alisema Bw.Geoffrey Mwambe Mkurugenzi Mtendaji wa TIC.

“Abiria wa kigeni akitua Tanzania kitu cha kwanza atakachokutana nacho ni sura ya nchi ambayo inatambulishwa na uwanja wa ndege mzuri, sisi Tanzania tupo vizuri! Napenda kuishukuru serikali ya awamu ya tano ya Rais Magufuli kwa kuimarisha miundombinu, tumeona hivi karibuni Rais akizindua barabara ya juu ya Mfugale,tunaona kasi ya ujenzi wa reli ya Standard Gauge, ujenzi wa uwanja huu na mengineyo mengi,kwetu sisi TIC tumefarijika kwani wawekezaji sasa watapata urahisi wa usafirishaji” Alisema Mwambe, Mkurugenzi Mtendaji wa TIC.

Jengo hilo jipya la tatu la uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere,  litahusika na  ndege za kimataifa tu na litahudumia abiria milioni 6 kwa mwaka, na kuwa na uwezo wa kuhudumia abiria hata 2,800 kwa saa kwa wanaoingia na kutoka,  na pia utahudumia ndege kubwa 19 na ndege ndogo 11 zinazoingia na kutoka nchini  kwa wakati mmoja.

Ujenzi wa Jengo la tatu (Terminal 3) JNIA ulioanza Juni, 2013 na utakaogharimu jumla ya Shilingi Bilioni 560 unakabidhiwa rasmi mamlaka husika tayari kwa kuutumia Mei, 2019 ukiwa katika viwango vyote vya kimataifa na kwa sasa wajenzi wanasema kazi ilyosalia ni ndogo ya asilimia 17.

Tags: Geoffrey MwambeTAATICujenziUwanja wa ndegeuwekezaji
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu.

Mgalu ashauri wananchi kuchangamkia umeme

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In