• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Monday, January 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Stiegler’s Gorge njia sahihi kufikia uchumi wa viwanda-Rais Magufuli

Serikali ipo imara na itahakikisha mradi huo unaotarajiwa kuzalisha Megawati 2,100 unakamilika kwa wakati ili kuiwezesha Tanzania kuweza kupiga hatua kubwa zaidi kimaendeleo.

Patricia Richard by Patricia Richard
December 13, 2018
in NISHATI
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi mara baada ya kushuhudia tukio la kihistoria la utiaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji ambao utagharimu zaidi ya kiasi cha Shilingi za kitanzania Trilioni 6

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi mara baada ya kushuhudia tukio la kihistoria la utiaji saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2100 katika mto Rufiji ambao utagharimu zaidi ya kiasi cha Shilingi za kitanzania Trilioni 6

Share on FacebookShare on Twitter

Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli ameihakikishia serikali ya Misri kuwa serikali ya awamu ya tano itasimamia utekelezaji wa mradi wa kuzalisha umeme katika Mto Rufiji (Stiegler’s Gorge) kwani mradi huo ni njia sahihi ya kufikia uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025. Rais Magufuli amesema hayo wakati akizungumza katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa mradi huo Ikulu jijini Dar es Salaam, zoezi lililoshuhudiwa na Waziri Mkuu wa Misri, Dk. Mostafa Madbouly.

Rais Magufuli ameeleza kuwa serikali yake ipo imara na itahakikisha mradi huo unaotarajiwa kuzalisha Megawati 2,100 unakamilika kwa wakati ili kuiwezesha Tanzania kuweza kupiga hatua kubwa zaidi kimaendeleo. Rais Magufuli amesema imekusudia kuharakisha utekelezaji wa mradi wa Stiegler’s Gorge kutokana na kwamba, uzalishaji wa umeme kupitia chanzo cha maji ni rahisi ukilinganisha na vyanzo vingine vya uzalishaji wa nishati ya umeme ikiwemo upepo, makaa ya mawe, nyuklia, jua na joto ardhi.

ADVERTISEMENT

“Ukiutazama mradi huu wa Stiegler’s Gorge unatoka katika mikoa na maeneo ambayo yana kiasi kikubwa cha mvua, lakini pia umeme wa maji ni rahisi sana ni Tsh 36 kwa uniti moja ukilinganisha na Nyuklia (Tsh 65), Jua (Tsh 103.5), joto ardhi (Tsh 114.5), upepo (Tsh 103.5), Makaa ya Mawe (Tsh 118), na mradi huu ukikamilika bei ya umeme itashuka kwa kiasi kikubwa sana”. Amesema Rais Magufuli.

Kuhusu tuhuma kutoka kwa baadhi ya  makundi ya watu kuwa mradi huo utaleta tishio la uharibifu wa mazingira katika hifadhi ya Selous, Rais Magufuli amesema jambo ambalo halina ukweli wowote.

“Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na timu ya watalaamu wa serikali, hakutokuwa na athari yoyote ya mazingira na kwa kuwa mradi wote unachukua asilimia 1.8 ya eneo la hifadhi, lakini  eneo lile litakuwa eneo mahususi kwa wanyama, ndege na viumbe wote wa majini ikiwemo kuongezeka kwa mazalia ya samaki”. Ameeleza Rais Magufuli.

 

Tags: MagufulimisriStiegler's Gorgeumemeuzalishaji
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
USDF yawapa tumaini wakulima kahawa

Wakulima walilia malipo Mbeya

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In