• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Thursday, March 30, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

Biashara ya Bodaboda: Baraka au Majanga?

Patricia Richard by Patricia Richard
May 16, 2018
in BIASHARA, UJASIRIAMALI
0
Share on FacebookShare on Twitter

Biashara ya pikipiki maarufu kama ‘bodaboda’ imekuwa moja kati ya biashara ambazo zimekuja kwa kasi sana kote nchini. Ukilinganisha na miaka kumi nyuma usafiri huu umekuja kwa kasi na kuteka soko kwa kiasi kikubwa sana. Zamani watu walitegemea usafiri wa daladala, bajaji na taxi ili kufika watakapo lakini hali imekuwa tofauti hivi sasa. Wengi wamekuwa wakikimbilia usafiri huu kwa sababu ni wa haraka na unaokoa muda kwani hutumii muda mrefu kusubiri foleni kama ilivyo kwa magari.

Tukiangazia usafiri huu kibiashara, umekuwa neema kwa watu wengi hasa vijana kwani wengi wameweza kujiajiri au kuajiriwa hivyo umepunguza tatizo la ajira kwa kiasi kikubwa sana. Hivi sasa vijana wengi wamekuwa wakijishughulisha na uendeshaji bodaboda na kujiingizia kipato. Kwa upande wa wananchi, usafiri huu umerahisisha shughuli mbalimbali za kiuchumi kwani umekuwa nafuu na watanzania walio wengi wanaweza kumudu gharama zake. Pia unaokoa muda hivyo mtu anaweza kufanya shughuli nyingi zaidi na kufikisha huduma mbalimbali hata sehemu za mbali ndani ya muda mfupi.

ADVERTISEMENT

Biashara hii pia ni uwekezaji mzuri ambao hauhitaji mtaji mkubwa sana hivyo watu wengi wanaweza wakafanya. Biashara hii inalipa kwa sababu haiangalii muda, msimu wala aina fulani ya watu katika jamii. Kila mtu ni mteja hivyo faida yake ni kubwa kama utapata dereva  muaminufu na mahesabu yako yataenda vizuri. Unaweza kuanza biashara hii na pikipiki moja na kuikuza biashara yako kutokana na faida utakayopata. Hivyo uwekezaji huu ni njia rahisi ya kujiingizia kipato endapo ukiwa makini.

Japokuwa biashara hii inakuja na neema lukuki, ina majanga yake katika jamii. Athari kubwa ambayo imezaliwa kutokana na ukuaji wa biashara ya bodaboda ni vifo au ulemavu wa kudumu. Madereva wengi wa bodaboda hawafanya mafunzo ya udereva, hawamiliki leseni, hawana uelewa wa kutosha kuhusu kanuni na sheria za barabarani na hivyo husababisha ajali nyingi hapa nchini. Wengi wamekuwa wakijiingiza katika fani hii kwa mazoea bila kufikiria kuwa wanahatarisha maisha ya watu kila wakiwa barabarani.

Pia uwepo wa biashara ya bodaboda umepelekea ongezeko kubwa la matukio ya uhalifu katika jamii. Baadhi ya madereva wa pikipiki wamekuwa sio waaminifu na wamekuwa wakishirikiana na majambazi ili kupora wananchi mali zao. Biashara hii imekuwa sio ya kuaminika kwani wengi wamekuwa wakiona madereva kama maadui zao japokuwa kuna baadhi ni waaminifu na biashara zao huathiriwa kutokana na matendo ya wenzao wachache.

Ili kufanya biashara hii kuwa endelevu na kubadilisha maisha ya wengi kiuchumi ni vizuri kama itafanywa katika utaratibu sahihi. Madereva wapate mafunzo sahihi ya kutumia vyombo vya moto na kupatiwa leseni na taasisi husika, kanuni na sheria za barabarani zifatwe na waendesha bodaboda wasiweke maisha ya abiria wao hatarini.

Tags: biasharaBodabodauwekezaji
Patricia Richard

Patricia Richard

Next Post
Fahamu haya kuhusu viwango vya riba

Jinsi ya kufungua akaunti ya benki

Discussion about this post

Habari Mpya

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

March 30, 2023
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

March 28, 2023
Lusaka-Zambia. Picha|Mtandao

Watanzania watakiwa kuchangamkia fursa Zambia

March 27, 2023
Waziri  wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa, Adolf Mkenda.

Waziri wa Elimu azungumza na Benki ya Dunia

March 27, 2023

Bilioni 647.5 kuitoa Kagera gizani

March 17, 2023
Waziri wa Fedha na Mipango Mwigulu Nchemba.

44.4bn kutumika matumizi ya kawaida na maendeleo

March 13, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Serikali, Benki ya Dunia wajadili ushiriki Sekta binafsi

by Pesatu Reporter
March 30, 2023
0

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru amesema Serikali inafanya majadiliano ya kimkakati na Benki ya Dunia...

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Msiwabanie vijana wajasiriamali: Majaliwa

by Pesatu Reporter
March 28, 2023
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza viongozi wa Mkoa wa Simiyu wasiwabane wajasiriamali, wawaelimishe na kuwapa miongozo ili wajiendeleze kiuchumi. Majaliwa...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In