• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, January 29, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

JE UNA KADI ZA BIASHARA?,SOMA KUJUA UMUHIMU WAKE

Wafanyabiashara bado wana nafasi kubwa ya kukuza mitandao yao kwa kubadilishana kadi.

Jensen Kato by Jensen Kato
May 28, 2020
in BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Kadi zimekuwa muhimu sana kwa wafanyabiashara hususani katika suala zima la kukuza mtandao wa biashara zao. Kadri muda unavyokwenda na uboreshwaji wa teknolojia za mawasiliano kadi za biashara zimeonekana kupoteza umuhimu wake kwa kiasi kikubwa na kuwafanya wafanyabiashara wengi kutokuwa nazo.

Ikiwa wewe ni mfanyabiashara unatakiwa kutambua kuwa kadi ni muhimu wakati wowote kwa sababu zifuatazo:

Teknolojia zimerahisishwa kwa kiasi kikubwa na hivi sasa inawezekana kusambaza habari mbalimbali kutoka katika simu moja kwenda nyingine ili mradi watumiaji wote wawe wanatumia simu za aina moja. Hivyo hata kama unaweza kubadilishana habari zako za mawasiliano na mteja ambaye anatumia simu kama chako haimaanishi itawezekana kwa kila mteja. Ili kurahisisha mawasiliano, tengeneza kadi za biashara na kumpatia kila mteja ambaye utawasiliana naye.

Sio kila mtu anatumia smartphone na mwenye uelewa wa kupata mawasiliano katika mitandao ya kijamii. Ili kurahisisha utoaji wa mawasiliano kwa wateja ni vyema kuwafikiria wale wasiotumia mtandao. Hii itawavutia kununua bidhaa kila watakapoihitaji kupitia mawasiliano yaliyopo katika kadi ya biashara yako.

ADVERTISEMENT

Kadi zinaweza kutumika hata katika maeneo ambayo hakuna mtandao kama kijijini au sehemu ambazo hairuhusiwi kutumia simu kama vile kwenye ndege au hospitalini. Kwa kutoa kadi ya biashara unawapa wateja uhakika wa kukupata kirahisi.

Kadi ya biashara huongeza uhalali kwenye biashara. Siku zote watu hupendelea zaidi kujihusisha na biashara ambazo zinaaminika. Kuwa na kadi kutawaaminisha wateja kuhusu huduma zako na umakini ulionao hivyo kununua bidhaa zako kwa uhuru zaidi.

Kwa kugawa kadi za biashara ni dhahiri kuwa unakuza biashara yako kwani mteja husika baada ya kufurahishwa na huduma au bidhaa zako atatumia mawasiliano uliyompa kwa watu wengine ili nao waweze kujipatia bidhaa au huduma. Ni muhimu kuweka habari zote muhimu kuhusu biashara yako katika kadi yako ya biashara.

Mitandao imeendelea kuleta mafanikio makubwa lakini wafanyabiashara bado wana nafasi kubwa ya kukuza mitandao yao kwa kubadilishana kadi ili kuweza kupeana fursa mpya za kibiashara na uwekezaji, kubadilishana ujuzi na uzoefu na kuongeza mauzo katika biashara.

Jensen Kato

Jensen Kato

Next Post

NI IPI MIPANGO YA FEDHA YAKO?

Discussion about this post

Habari Mpya

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

January 26, 2023

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

January 21, 2023

Serikali kuanzisha mnada wa chai

January 20, 2023

Tumieni bandari ya Dar es Salaam: Makalla

January 19, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan akizungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani.

Sekta ya kilimo kukua kwa 10% 2030: Rais Samia

January 19, 2023

Ndege tano kuwasili mwaka huu

January 17, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Poland kuisaidia Tanzania kuweka mifumo ya kodi kidigitali

by Pesatu Reporter
January 26, 2023
0

Poland imeahidi kuisadia Tanzania kuimarisha mifumo ya kodi kwa njia ya kidigitali ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya...

Kamati ya bunge yahimiza uwekezaji maeneo ya hifadhi

by Pesatu Reporter
January 21, 2023
0

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeishauri Wizara ya Maliasili na Utalii iendelee kuzifanyia maboresho kanuni...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In