• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Saturday, September 23, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

NI IPI MIPANGO YA FEDHA YAKO?

Jensen Kato by Jensen Kato
May 29, 2020
in FEDHA, Uncategorized
0
Share on FacebookShare on Twitter

Je, unajua nini unataka kufanya na fedha zako? Kama bado hufahamu basi tambua kuwa una hatari ya kutumia fedha hizo bila mpangilio. Siku zote kuwa na mpango husaidia kufanikisha mambo makubwa. Ni muhimu kujua kwamba huwezi kutimiza malengo yote uliyonayo na ili kufanikiwa, ni muhimu kuwa na malengo madhubuti ambayo hata ukiwekeza fedha zako, utafaidika.

Ni vyema kukumbuka kuwa, ni rahisi kuweka malengo lakini ni ngumu sana kuyatimiza kwa sababu maneno na matendo ni mambo mawili tofauti. Yafuatayo yanaweza kukusaidia kutambua malengo yako na kuyatimiza:

Jiwekee malengo: Tambua kuwa una mamlaka ya kuweka malengo ya aina yoyote unayotaka ili mradi tu uwe unaamini katika malengo hayo. Ikiwa hujiamini hakuna mtu mwingine atakayekuja kukusaidia kuyaamini malengo hayo na hata kama itatokea, ni mchakato mgumu kwako na kwa wale wanaokusaidia kwani tangu mwanzo hukuwa na imani na malengo hayo. Chukua muda kutafakari mambo ambayo yana umuhimu kwako kisha chagua machache unayoweza kuyafanyia kazi.

Hakikisha una malengo maalum na yanayopimika: Unapoweka malengo yako ni muhimu kuwa na maelezo ya kutosha juu ya yale unayotarajia kutimiza hivyo hakikisha unafafanua haswa maana ya mafanikio katika malengo husika.

Weka malengo yenye busara na maana: Kuweka malengo ambayo unajua kabisa huwezi kufanikisha kutasababisha ushindwe na upoteze muda wako kwa mambo yasiyowezekana. Unapojiwekea malengo maalum, yanayoweza kupimika, hakikisha unaweza kuyafikia malengo hayo. Hivyo unaweza kuwa malengo ambayo yanaweza kuonekana ni madogo lakini utakapoyatimiza, utapata moyo wa kufikia malengo makubwa zaidi.

ADVERTISEMENT

Gawa malengo: Kutimiza malengo makubwa kunaweza kukatisha tamaa watu wengi kwa sababu ya muda mwingi ambao hutumia. Ili kuendelea kuhamasika kukamilisha malengo yako, gawanya malengo hayo katika mafungu madogo madogo kisha chagua malengo ambayo unaweza kukamilisha kwa wakati unaofaa.

ADVERTISEMENT

Tenga muda: Katika kila lengo unatakiwa kuwa na tarehe ya mwisho ya kukamilisha lengo husika ili kuepuka kutumia muda mwingi katika jambo moja. Kuwa na ratiba kutakuruhusu kufuata mafanikio yako kwa urahisi zaidi na kuhakikisha upo kwenye njia sahihi. Jitahidi kuweka muda usiozidi mwaka ili kujua kila mwaka umefikia wapi na ni lengo gani linatakiwa kupewa kipaumbele zaidi.

Fuatilia maendeleo yako: Mwisho ni muhimu kujua muelekeo wa juhudi zako ili kufikia malengo yako kwa kufanya hivyo itakurahisishia kufanya marekebisho ikiwa yanahitajika. Unaweza kutengeneza jedwali ili kurahisisha ufuatiliaji.

Jiwekee malengo leo na anza kufanikiwa kwa kuyatekeleza. Mawazo pekee hayatoshi hivyo wekeza nguvu na muda wa kutosha ili kutimiza ndoto zako.

Jensen Kato

Jensen Kato

Next Post

SIFA TANO ZA MJASILIAMALI BORA

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

September 14, 2023

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

September 14, 2023
Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande.

Tanzania yapiga hatua utakatishaji fedha

September 12, 2023
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Picha| Ikulu

Tutawaunganisha wakulima na soko: Rais Samia

September 11, 2023

Mbaazi yaleta neema kwa wakulima 2023

September 7, 2023

Bei za mafuta zapanda tena Tz

September 6, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Tanzania ni nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali barani Afrika na inashika nafasi ya 14 dunia. Ethiopia, ndio nchi...

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Benki ya Exim imezindua ushirikiano wa kimkakati na Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na kufanya mafunzo ya...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In