• Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
Sunday, September 24, 2023
  • Login
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI
No Result
View All Result
Pesatu
No Result
View All Result

SABABU ZA BIASHARA NYINGI KUKOSA WATEJA.

Wafanyabiashara wanatakiwa kubadilika kama wanataka kupata maendeleo.

Jensen Kato by Jensen Kato
June 17, 2020
in BIASHARA
0
Share on FacebookShare on Twitter

Ni muhimu kuwa makini katika kila jambo kwa sababu maamuzi yote huwa na matokeo mbeleni. Kwa upande wa biashara, wafanyabiashara wanashauriwa kuwa makini katika kila jambo kwani wateja huwa makini na kila kitu na kutokana na mtazamo wao wanaweza kuamua kuwa wateja wa kudumu au kutafuta sehemu nyingine ya kujipatia huduma wanayohitaji.

Haya ni baadhi ya mambo yanayoweza kupelekea kupoteza wateja katika biashara

Mazoea – Ili kuwavutia wateja wengi zaidi katika biashara yako ni muhimu kuwa mbunifu na mtu ambaye haogopi kufanya mabadiliko inapobidi. Wateja wengi hawafurahishwi na wafanyabiashara wanaofanya biashara kwa mazoea. Hili ni tatizo kubwa kwa wafanyabiashara wengi na hali hii inaathiri biashara taratibu na inaweza kusababisha biashara isiendelee kwa sababu wateja wataenda kununua bidhaa kwa mfanyabiashara ambaye yuko tayari kufanya vitu tofauti na mazoea yake ya kila siku.

Muda wa kufungua – Kwa ujumla hakuna mtu anayependa kupoteza muda au kucheleweshwa. Ikiwa mfanyabiashara ana tabia ya kuchelewa kufungua biashara yake ili hali anajua kuwa mahitaji ya wateja wake huanza mapema zaidi basi ni rahisi kukosa wateja hata wale wa kudumu kwa sababu mtu akiwa na uhitaji wa huduma au bidhaa huwa anataka kuipata kwa muda muafaka hivyo ikiwa mteja anakuta pamefungwa basi atatafuta sehemu nyingine ambayo anaweza kupata huduma husika na kutengeneza mazoea ya kwenda huko kila akiwa na uhitaji.

ADVERTISEMENT

Kukosa umakini – Kuna baadhi ya wafanyabiashara si makini na biashara zao kutokana na hilo hata wateja hupungua kwa sababu mteja siku zote hufurahishwa na mtoa huduma au mfanyabiashara makini, asiye na mambo mengi na anayejua umuhimu wa huduma bora kwa mteja. Kwa mfano mfanyabiashara ambaye kila mteja akija lazima atafutwe kwa sababu anashindwa kutulia katika biashara yake, ni dhahiri wateja watachoka na kutafuta sehemu nyingine yenye bidhaa au huduma unayotoa ili waweze kuendelea na mambo mengine. Au mfanyabiashara ambaye anatumia muda mrefu kwenye simu yake badala ya kumsikiliza mteja na kuhakikisha amepata huduma anayostahili lazima akose wateja kwani tabia hii haiwafurahishi watu.

Lugha – Kama mfanyabiashara lugha yako kwa wateja inaweza kupelekea ujipatie wateja wengi zaidi au la. Kwa sababu wateja wanaokuja katika biashara yako ni wa aina mbalimbali na wanakuwa wametoka kupitia mambo mbalimbali hadi kufika katika biashara yako. Mteja ana uwezo wa kuchagua sehemu yoyote anayotaka kwa ajili ya kununua bidhaa hivyo akipokelewa na lugha mbaya ni rahisi kwake kutafuta sehemu nyingine.

Wafanyabiashara wanatakiwa kubadilika kama wanataka kupata maendeleo kwani lengo la biashara ni kukuza uchumi. Jambo la msingi la kukumbuka ni kuwa mteja ana uhuru wa kuchagua ni wapi anataka kununua huduma au bidhaa hivyo ushindani ni mkubwa sokoni na wafanyabiashara wanapaswa kubadilika ili kujenge uaminifu kwa wateja wao.

ADVERTISEMENT
Jensen Kato

Jensen Kato

Next Post

TANESCO YAJIPANGA KUVUNA MABILIONI MKOA WA GEITA

Discussion about this post

Habari Mpya

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

September 14, 2023

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

September 14, 2023
Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande.

Tanzania yapiga hatua utakatishaji fedha

September 12, 2023
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Picha| Ikulu

Tutawaunganisha wakulima na soko: Rais Samia

September 11, 2023

Mbaazi yaleta neema kwa wakulima 2023

September 7, 2023

Bei za mafuta zapanda tena Tz

September 6, 2023

KUHUSU SISI

PesaTu ni kitengo cha habari cha MediaPix ambacho huandika makala za biashara na uchumi wa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Waasisi wa kampuni wana uzoefu mkubwa kwenye tasnia ya habari na mawasiliano wakiwa kwenye fani hio tangu mwaka 1905. PesaTu inamlenga kila mtu ambaye kwa namna moja au nyingine anaguswa na anapenda kujua/ kufuatilia masuala mbalimbali ya kiuchumi ya nchi ikiwemo ujasiriamali, uwekezaji, viwanda, kilimo na hisa.

LATEST

Waziri wa Maliasili na Utalii Angellah Kairuki.

Wadau ufugaji nyuki watakiwa kuchangamkia fursa

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Tanzania ni nchi ya pili kwa uzalishaji wa asali barani Afrika na inashika nafasi ya 14 dunia. Ethiopia, ndio nchi...

Benki ya Exim yajikita uwazi shughuli za bima

by Pesatu Reporter
September 14, 2023
0

Benki ya Exim imezindua ushirikiano wa kimkakati na Mamlaka ya Udhibiti wa Bima Tanzania (TIRA) pamoja na kufanya mafunzo ya...

RECOMMENDED

Waziri Mwijange aja na orodha ya viwanda visivyofanya kazi

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

  Na Mwandishi wetu. Baada ya Rais John Magufuli kuonyesha kukerwa na kitendo cha Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji...

Nane Nane itumike kama darasa huru kwa wakulima

by Patricia Richard
March 23, 2018
0

Na Mwandishi wetu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) imejitolea kuwapa mafunzo ya siku moja wakulima mkoani Lindi...

No Result
View All Result
  • Home
  • FEDHA
    • MIKOPO
    • BIMA
    • HISA
  • BENKI
  • BIASHARA
    • UJASIRIAMALI
    • UWEKEZAJI
    • BIASHARA NDOGO NDOGO
  • VIWANDA
    • MIUNDOMBINU
    • NISHATI
    • UZALISHAJI
  • KILIMO
    • KILIMO BIASHARA
    • KILIMO UFUNDI
  • MAHOJIANO
  • AFRIKA MASHARIKI
    • BIASHARA
    • FEDHA
    • UJASIRIAMALI

© 2023 JNews - Premium WordPress news & magazine theme by Jegtheme.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In